Ajabu mtu kuteswa kwa sababu ya kuwa na dini tofauti na wenzake- Guterres
Kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa hii leo kumefanyika mkutano wa 8 wa jukwaa la ustaarabu la Umoja wa Mataifa ambapo Katibu Mkuu Antonio Guterres ameelezea kustaajabu kwake jinsi tofauti ya imani ya kidini na tamaduni vinavyoendelea kuwa chanzo cha mauaji na mateso kwa baadhi ya wakazi wa dunia.