Lacroix awajulia hali majeruhi wa Tanzania waliolazwa Uganda
Mkuu wa operesheni za ulinzi za Umoja wa Mataifa Jean-Pierre Lacroix amewajulia hali walinda amani wawili wa Tanzania waliolazwa katika hospital ya Mulago mjini Kampala nchini Uganda.
Walinda amani hao wanapatiwa matibabu baada ya kujeruhiwa wakati wa shambulio huko Semuliki, Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC Alhamisi ya wiki iliyopita.
Akiwa wodini kuzungumza na majeruhi hao kuwajulia hali, mmoja wao amesema..
(Nats)
Na ndipo Bwana Lacroix akasema..
(Sauti ya Jean-Pierre Lacroix)
« Nimetoka idara ya ulinzi wa amani ya Umoja wa Mataifa, New York, nimekuja kuwajulia hali na kusema asante sana kwa huduma yenu. Nakutakia kila la kheri. »
Baada ya kutoka Mulago nchini Uganda, Bwana Lacroix ameelekea jijini Dar es salaam nchini Tanzania ambako kesho atahudhuria tukio maalum la kuaga miili ya walinda amani 14 waliouawa huko DRC.