Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

DR Congo

Kikundi cha utamaduni cha walinda amani kutoka Tanzania kikifanya onesho kwenye mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.
TANZBATT 7/Ibrahim Mayambua

TANZBATT-7 yatumia sanaa kuimarisha amani DRC

Sanaa katika operesheni za ulinzi wa amani zinazofanywa na Umoja wa Mataifa kwenye mataifa mbalimbali ikiwemo Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC imedhihirika  kuwa mbinu muhimu ya kuleta utangamano miongoni mwa wanajamii wa taifa hilo hususan jimboni Kivu Kaskazini kwa kuwa na ujumbe maridhawa wa amani kwa rai na kusahau magumu wanayopitia  kufuatia machafuko yaliyodumu kwa miongo kadhaa.

 

Sauti
3'11"
Ugawaji wa chakula na WFP kwa Watu waliohamishwa makao huko Kikuku, Kivu Kaskazini,  nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
WFP/Ben Anguandia

Watu 4 kati ya 10 nchini DRC hatarini kukosa chakula, msaada zaidi unahitajika- WFP

Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula WFP hii leo mjini Kinshasa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC limeonya kuwa kutokana na hali ya mgogoro pamoja na virusi vya corona vinavyoendelea kuongezeka nchini humo DRC na hivyo kuzidisha moja ya janga kubwa la njaa duniani na ambalo linapata ufadhili mdogo, mamilioni ya watu wanaweza kupoteza maisha ikiwa jumuiya ya kimataifa haitaingilia kati na usaidizi zaidi. 

Kamanda wa kikosi cha Tanzania huko DRC, Luteni Kanali John Ndunguru (katikati) katika mazungumzo na afisa wa jeshi la DRC, FARDC huko Beni, DRC.
TANZBATT 7/Ibrahim Mayambua

Saa 24 za mlinda amani TANZBATT 7 nchini DRC 

Kila mara tumekuwa tukimulika shughuli za jumla za walinda amani wa Umoja wa Mataifa wanaohudumu katika maeneo mbali mbali duniani iwe ni ujenzi wa barabara, ulinzi wa amani na hata kilimo lakini leo tunaangazia je mlinda amani mmoja mmoja siku yake inakuwa vipi? Na leo tunammulika Luteni Kanali John Ndunguru, Kamanda wa kikundi cha 7 cha Tanzania, TANZBATT 7, kwenye kikosi cha kujibu mashambulizi, FIB cha ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO. Anayetuletea ripoti hiyo ni Issa Mwakalambo, Afisa Habari wa TANZBATT 7. 

 

Sauti
2'8"