Ni sawa kuzipatia nchi misaada ya maendeleo lakini pia tuzijengee uwezo zijikwamue- Guterres
Mkutano wa Nne wa uchangishaji fedha kwa ajili ya maendeleo, FfD umeanza leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani ambapo Katibu Mkuu António Guterres amesema, “tunahitaji fedha zaidi ili kutekeleza na kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs.”