Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Burundi

Rangi ya buluu iliangaza ndani ya ukumbi wakati wa maadhimisho ya miaka 30 ya mkataba wa kimataifa wa haki za mtoto, CRC.
UN Photo/Manuel Elías

Rangi ya buluu ikitawala, Beckham asema "siku zijazo ni za watoto wetu hivyo tutunze ndoto zao"

Mustakabali si wa kwetu bali ni wa watoto wetu kwa hiyo tuchukue hatua zaidi kulinda ndoto za watoto, amesema David Beckham, Balozi mwema wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, wakati akihutubia hii leo kikao cha ngazi  ya  juu cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani kilichofanyika kuadhimisha miaka 30 tangu kupitishwa kwa mkataba wa haki za mtoto, CRC na sambamba na siku ya mtoto duniani,