Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Makala Maalum

Mtoto mwenye ulemavu wa ngozi tena mwenye ulemavu wa kutoona akisoma kwa kupitia maandishi maalum ua nukta nundu kwa watu wasioona au wenye uoni hafifu
© UNICEF/Pirozzi

Utafiti na Ushahidi juu ya Watoto wenye Ulemavu: UNICEF

Ingawa Malengo ya Maendeleo Endelevu yanahimiza kuwa hakuna mtoto anayepaswa kuachwa nyuma. Lakini utafiti uliofanywa na Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumiwa watototo UNICEF unaonesha kuwa kati ya watoto milioni 240 wenye ulemavu duniani, nusu hawajawahi kuhudhuria shule, takriban theluthi moja hawapati chakula bora na chakutosha na pia watoto wenye ulemavu wanawakilishwa kwa njia isiyo sawa na wengi wao wanaachwa nyuma. 

Mpaka wa Burundi na DR Congo. UNHCR inawasaidia wakimbizi wa Burundi waliokuwa DR Congo kurejea nyumbani.
Screenshot

Waliokuwa wakimbizi nchini DRC wafurahia kurejea nyumbani Burundi  

Raia 272 kutoka familia 78 wa Burundi waliorejea nchini Burundi kutoka kambi ya wakimbizi ya Lusenda katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo mwishoni mwa wiki iliyopita wamekaribishwa na wanachi wenzao, serikali na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi ili waanze maisha katika nchi yao waliyoikimbia kwa vipindi tofauti kutokana na hali mbaya ya usalama