Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Makala Maalum

Shamba la mmea wa tumbaku nchini Kenya
© WHO

FAO yawasaidia wakulima wa tumbaku Kenya, kuhamia katika mazao mbadala

Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO limeimarisha afya ya wakulima wa kaunti ya Migori. Hii ni baada ya kuzindua machi Mwaka huu mradi wa kilimo mbadala unaolenga kusitisha kile cha tumbaku. Kwa ushirikiano wa WHO na WFP, FAO inajivunia mafanikio kwani afya za wakulima wa Migori zimeimarika baada ya kuacha kilimo cha tumbaku na kukiongeza kipato chao.

Esperance Tabisha ajulikanaye pia kama Esperanza akiwa nje ya makazi yao mapya huko Ontario Canada na ni kutokana na programu ya mkimbizi kuhamia nchi ya tatu chini ya mkataba wa kimataifa wa wakimbizi wa mwaka 2018.
UN News Video

Esperance Tabisha: Kutoka kuwa mkimbizi Kakuma hadi mbunifu wa mitindo Canada

Esperance Tabisha, raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambaye sasa ni mnufaika wa mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu wakimbizi, GCR uliopitishwa mwaka 2018 wenye vipengele kadhaa ikiwemo kuhamishia wakimbizi nchi ya tatu. Alikimbia vita DRC na kuingia kambi ya Kakuma nchini Kenya mwaka 2010 na mwaka 2019 akahamia Canada kupitia msaada wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR.