Kupigania haki za binadamu ni jukumu linaloendelea: Bachelet
Kamishina mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Michelle Bachelet anahitimisha muhula wake mamlakani kesho Jumatano 31 Agosti baada ya kuhudumu katika wadhifa huo kwa miaka minne.
Kamishina mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Michelle Bachelet anahitimisha muhula wake mamlakani kesho Jumatano 31 Agosti baada ya kuhudumu katika wadhifa huo kwa miaka minne.
Wataalamu huru wa haki za binadamu walioteuliwa na Umoja wa Mataifa leo wametoa wito wa kuchukuliwa hatua kali zaidi za kuzuia na kuadhibu vitendo vya ukeketaji wa wanawake nchini Sierra Leone.
Katika Siku ya usaidizi wa kibinadamu Duniani, inayoadhimishwa kila mwaka tarehe 19 Agosti, wafanyakazi wa misaada Ahmad Alragheb, anayeishi nchini Syria, na Veronica Houser, aliyeko Afghanistan, wanazungumza kuhusu juhudi muhimu za kibinadamu katika nchi hizi, na changamoto wanazokabiliana nazo wao na wenzao.
Kila siku asubuhi na mapema kukipambazuka na jua kuchomoza Rahot mwenye umri wa miaka 55 huamka na kumbeba mgongoni mjukuu wake Hassan tayari kwakuaza safari ya takriban kilometa 20 yenye vilima kwenda kituo cha kumpatia lishe mjukuu huyo ili kuokoa maisha yake kutokana na kuwa na utapiamlo mkali.
Kutoka Ethiopia hadi Chad na Palestina, Elimu haiwezi kusubiri au ECW , ni mradi wa Umoja wa Mataifa wa elimu katika maeneo yenye dharura na migogoro ya muda mrefu, ambao umesaidia mamilioni ya wavulana na wasichana walioathiriwa na migogoro duniani kote kutimiza ndoto zao.
Sam Aderubo alianzisha kampuni yake, Honey Pride, huko Arua, kaskazini mwa Uganda, ili kuleta matokeo chanya kwa jamii yake. Kwa msaada kutoka kwa Umoja wa Mataifa, biashara inashamiri, ikitoa kazi kwa mamia ya wafugaji nyuki wa ndani, ambao wengi wao ni wanawake na vijana waliotengwa.
Takribani vijana mia saba, kwa takribani wiki 6, wamekuwa katika vuo vikuu mbalimbali nchini Marekani wamesafiri kupata maarifa ya uongozi kupitia Mpango wa serikali ya Marekani unaolenga kuwaelimisha viongozi vijana wa Afrika ili waweze kuwa viongozi bora katika jamii zao.