Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Makala Maalum

Mwanamke mzee akiwa katika kambi ya wakimbizi wandani nchini Somalia
© UNICEF/Sebastian Rich

WHO yatoa vipaumbele 5 kukabiliana na unyanyasaji wa wazee

Leo ni siku ya kuhamasisha kupinga unyanyasaji dhidi ya wazee na katika kuadhimisha siku hii Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO na wadau wake wamechapisha vipaumbele vitano vitakavyosaidia kuzuia na kukabiliana na unyanyasaji wa wazee na hivyo kuchangia katika kuboresha afya, utawi na utu wao.

Wavuvi pwani ya Kenya.
UN News/Thelma Mwadzaya

Tusipoilinda bahari tunaathiri kizazi cha sasa na vijavyo: Wananchi wa Vanga Kenya 

Ikiwa leo ni siku ya bahari duniani Umoja wa Mataifa imeichagiza dunia kuchukua hatua Madhubuti ili kuhakikishwa inalindwa kwa ajili ya maslhai ya kizazi cha sasa na kijacho kwani bahari sio tu inahakikisha uhakika wa chakula kwa mamilioni ya watu , bali pia ni moja wa muajiri mkubwa na inachangia kwa kiasi kikubwa katika pato la dunia la kila mwaka.  

Watalaam, hudumu za kiafya wakati wa ujauzito na kujifungua zinaweza kuzuia Fistula.
© UNFPA Mozambique

Mambo 5 unayopaswa kufahamu kuhusu Fistula: UNFPA 

Fistula itokanayo na uzazi ni nini? 

Ni jeraha kubwa la wakati wa kujifungua ambalo humpokonya mwanamke au msichana afya yake, haki na utu.  

Ni shimo linalotokea kati ya njia ya uzazi na kibofu ambayo husababisha kutoweza kudhibitiwa kwa mkojo.  

Pia ni shimo kati ya njia ya uzazi na njia ya haja kubwa husababisha kinyesi kuvuja bila kujizuia.