WHO yatoa vipaumbele 5 kukabiliana na unyanyasaji wa wazee
Leo ni siku ya kuhamasisha kupinga unyanyasaji dhidi ya wazee na katika kuadhimisha siku hii Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO na wadau wake wamechapisha vipaumbele vitano vitakavyosaidia kuzuia na kukabiliana na unyanyasaji wa wazee na hivyo kuchangia katika kuboresha afya, utawi na utu wao.