Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Natiwa moyo na angalau kuwepo kwa misimamo ya pamoja baina ya pande kinzani Syria- Pedersen
Wajumbe wa pande kinzani nchini Syria wanaokutana mjini Geneva, Uswisi kwa lengo la kusaka suluhu ya kudumu na kumaliza mzozo wa takribani muongo mmoja nchini mwao, angalau wamekuwa na misimamo inayofanana itakayoweza kusongesha mbele majadiliano, amesema Geir Pedersen, Mjumbe Maalum wa Umoja wa Mataifa kwa mzozo wa Syria.
Tanzania tumeshinda tuzo na utalii umerejea– TTB
Wakati janga la ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 likiendelea kusababisha zahma kwingineko duniani na hata kukwamisha shughuli za kiuchumi na kijamii, nchini Tanzania hali ni tofauti, utalii umerejea na tuzo juu ya kimataifa, kulikoni? Stella Vuzo wa kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa, UNIC jijini Dar es salaam, Tanzania amemhoji Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii Tanzania, TTB, Devotha Mdachi.
UNDP yapigia chepuo uimarishaji wa sekta ya utalii Tanzania
Nchini Tanzania, shirika la mpango wa maendeleo la Umoja wa Mataifa, UNDP limeshiriki katika uzinduzi wa moja kati ya magari matatu ya magonjwa ambayo yatatumika katika hifadhi ya Taifa na mbuga za wanyama wakati huu ambapo taifa hilo la Afrika Mashariki limefungua tena milango yake kwa watalii wa nje na wa ndani.
Miongozo ya utalii imetuwezesha kushinda tuzo na utalii umerejea Tanzania – TTB
Wakati janga la ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 likiendelea kusababisha zahma kwingineko duniani na hata kukwamisha shughuli za kiuchumi na kijamii, nchini Tanzania hali ni tofauti na kutokana na kuzingatia kanuni za kulinda wananchi na watalii, shughuli za utalii zimerejea na hata taifa hilo la Afrika Mashariki limepata tuzo ya Mhuri wa kimataifa.
Mipango ya kudhibiti COVID-19 ilianza punde tu baada ya maambukizi kuripotiwa China, yasema Mauritius
Mauritius, taifa la kisiwani lililo katika bahari ya Hindi limeelezea kile kilicholiwezesha kudhibiti ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 punde tu baada ya kuthibitishwa kuwepo kwa wagonjwa 3 nchini humo. Ahimidiwe John Kibego na maelezo zaidi.
Fukwe katika mji mkuu wa Mauritius, Port Louis, zikionekana tupu bila wageni wowote wakati wa zama za mlipuko wa ugonjwa wa COVID-19 mwezi Machi mwaka huu wa 2020.
Mipango ya kudhibiti COVID-19 ilianza punde tu baada ya maambukizi kuripotiwa China, yasema Mauritius
Mauritius, taifa la kisiwani lililo katika bahari ya Hindi limeelezea kile kilicholiwezesha kudhibiti ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 punde tu baada ya kuthibitishwa kuwepo kwa wagonjwa 3 nchini humo mwezi Machi mwaka huu.
Uwezekano wa kuambukizwa COVID-19 kwa mara ya pili ni mdogo- WHO
Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO limesema kuna uwezekano mdogo sana kwa mtu kuambukizwa zaidi ya mara moja ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19.
COVID-19 imevuruga harakati za kukabiliana na ugaidi- Guterres
Leo ni siku ya kimataifa ya kukumbuka waathiriwa na manusura wa vitendo vya kigaidi ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres katika ujumbe wake amesema janga la COVID-19 linakwamisha harakati za kusaidia manusura wa ugaidi.
19 Agosti 2020
Jaridani la Umoja wa Mataifa hii leo na Flora Nducha
-Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya kibindamu na masula ya dharura OCHA yatoa shukrani zake kwa wahudumu wa kibinadamu kokote waliko katika kuokoa maisha.
- Ikiwa leo ni siku ya huduma za kibinadamu duniani Umoja wa Mataifa umesema unawaenzi wahudumu hao ambao wanakabiliana na changamoto lukuki katika kuokoa na kuboresha maisha ya mamilioni ya watu.