Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataif kwa Syria, Geir O.pedersen akizungumza na wanahabari. (PIcha ya maktaba)
UN Photo/Evan Schneider

Natiwa moyo na angalau kuwepo kwa misimamo ya pamoja baina ya pande kinzani Syria- Pedersen 

Wajumbe wa pande kinzani nchini Syria wanaokutana mjini Geneva, Uswisi kwa lengo la kusaka suluhu ya kudumu na kumaliza mzozo wa takribani muongo mmoja nchini mwao, angalau wamekuwa na misimamo inayofanana itakayoweza kusongesha mbele majadiliano, amesema Geir Pedersen, Mjumbe Maalum wa Umoja wa Mataifa kwa mzozo wa Syria.

 

World Bank/Curt Carnemark

Tanzania tumeshinda tuzo na utalii umerejea– TTB

Wakati janga la ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 likiendelea kusababisha zahma kwingineko duniani na hata kukwamisha shughuli za kiuchumi na kijamii, nchini Tanzania hali ni tofauti, utalii umerejea na tuzo juu ya kimataifa, kulikoni?  Stella Vuzo wa kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa, UNIC jijini Dar es salaam, Tanzania amemhoji Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii Tanzania, TTB, Devotha Mdachi.

 

Sauti
6'1"
Mwakilishi Mkazi wa UNDP nchini Tanzania, Christine Musisi akizindua moja ya magari ya wagonjwa ambayo yamebadilishwa kutoka magari ya kawaida kufuatia msaada wa fedha kutoka shirika hilo la UN.
UNDP/Sawiche Wamunza

UNDP yapigia chepuo uimarishaji wa sekta ya utalii Tanzania

Nchini Tanzania, shirika la mpango wa maendeleo la Umoja wa Mataifa, UNDP limeshiriki katika uzinduzi wa moja kati ya magari matatu ya magonjwa ambayo yatatumika katika hifadhi ya Taifa na mbuga za wanyama wakati huu ambapo taifa hilo la Afrika Mashariki limefungua tena milango yake kwa watalii wa nje na wa ndani.

Afisa wa mbuga ya taifa nchini Tanzania akipima joto la mtalii kama moja ya kanuni za kudhibiti ugonjwa wa COVID-19.
TTB Video screenshot

Miongozo ya utalii imetuwezesha kushinda tuzo na utalii umerejea Tanzania – TTB

Wakati janga la ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 likiendelea kusababisha zahma kwingineko duniani na hata kukwamisha shughuli za kiuchumi na kijamii, nchini Tanzania hali ni tofauti na kutokana na kuzingatia kanuni za kulinda wananchi na watalii, shughuli za utalii zimerejea na hata taifa hilo la Afrika Mashariki limepata tuzo ya Mhuri wa kimataifa. 

Sauti
6'1"
UN /Manuel Elias

Mipango ya kudhibiti COVID-19 ilianza punde tu baada ya maambukizi kuripotiwa China, yasema Mauritius

Mauritius, taifa la kisiwani lililo katika bahari ya Hindi limeelezea kile kilicholiwezesha kudhibiti ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 punde tu baada ya kuthibitishwa kuwepo kwa wagonjwa 3 nchini humo. Ahimidiwe John Kibego na maelezo zaidi. 

Fukwe katika mji mkuu wa Mauritius, Port Louis, zikionekana tupu bila wageni wowote wakati wa zama za mlipuko wa ugonjwa wa COVID-19 mwezi Machi mwaka  huu wa 2020. 

Sauti
2'23"

19 Agosti 2020

Jaridani la Umoja wa Mataifa hii leo na Flora Nducha

-Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya kibindamu na masula ya dharura OCHA yatoa shukrani zake kwa wahudumu wa kibinadamu kokote waliko katika kuokoa maisha.

- Ikiwa leo ni siku ya huduma za kibinadamu duniani Umoja wa Mataifa umesema unawaenzi wahudumu hao ambao wanakabiliana na changamoto lukuki katika kuokoa na kuboresha maisha ya mamilioni ya watu.

Sauti
13'27"