Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
COVID-19 yaongeza machungu sekta ya utalii Kenya
Janga la ugonjwa wa virusi vya Corona, COVID-19 nchini Kenya limekuwa na athari kwa sekta ya uhifadhi wa wanyamapori na hivyo kuweka hatarini mustakabali wa wanyamapori kwenye hifadhi. Flora Nducha na ripoti kamili.
Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa, UNEP kupitia video yake limemulika hifadhi ya taifa ya Amboseli, kusini mwa Kenya ambayo tangu COVID-19 ikumbe taifa hilo katikati ya mwezi Machi mwaka huu,, imesababisha sekta ya utalii kudorora, wakazi jirani wa eneo hilo kukosa ajira na wanyama kukosa ulinzi.
Misaada ya kibinadamu pekee haitoshi kumaliza janga la njaa:IFAD
Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa maendeleo ya kilimo IFAD umesema misaada ya kibinadamu pekee haitoshi kushughulikia janga kubwa la njaa linaloizogoma dunia hivi sasa kunahitajika hatua za kuijengea jamii mnepo kukabili janga hilo
COVID-19 yaongeza machungu sekta ya utalii Kenya
Janga la ugonjwa wa virusi vya Corona, COVID-19 nchini Kenya limekuwa na athari kwa sekta ya uhifadhi wa wanyamapori na hivyo kuweka hatarini mustakabali wa wanyamapori kwenye hifadhi.
Unyonyeshaji kwa ajili ya dunia enye afya:UNICEF/WHO
Wiki ya unyonyeshaji duniani imeanza Agosti Mosi huku Umoja wa Mataifa ukizitaka jamii zote kila mahali “kuunga mkono unyonyeshaji kwa ajili ya kuwa na dunia yenye afya.”
COVID-19 bado ipo na athari zake zitakuwa za miongo:WHO
Kamati ya dharura ya shirika la afya duniani WHO ya kupambana na janga la corona au COVID-19 imekutana mjini Geneva Uswis katika kikao maalum kilichoitishwa na mkurugenzi mkuu wa shirika hilo Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus.
Tusipochukua hatua sahihi na kwa haraka, Amerika Kusini na Karibea watu watakufa- WFP
Shirika la Mpango wa chakula la Umoja wa Mataifa WFP limeonya kuwa kuongezeka kwa njaa, uchumi unaoyumba, ukosefu wa usawa na msimu wa vimbunga vikali, vinatishia watu wa Amerika Kusini na Karibea na vinaweza kuwa na athari zaidi kama hatua za haraka hazitachukuliwa.
WHO yasaidia kurejesha kwa madaktari wa Azerbaijan ili wasaidie mapambano dhidi ya COVID-19 nchini mwao
Ikiwa ni sehemu ya msaada wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO kwa harakati za Azerbaijan kupambana na virusi vya corona au COVID-19, mradi wa REACT-C19 umewaleta madaktari 19 raia wa Azerbaijan waliokuwa wanafanya kazi Uturuki ili warudi nyumbani kusaidia kutoa mafunzo kwa wafanyakazi wa sekta ya afya kuhusu jinsi ya kushughulikia COVID-19.
Hata kama corona imetuingilia, bado tunaamini bado maisha yako mbele-Wanafunzi wakimbizi Uganda
Makala ifuatayo inamulika changamoto wanazokumbana nazo wanafunzi wakimbizi ambao hivi sasa wanalazimika kusalia majumbani ndani ya kambi baada ya shule kufungwa nchini Uganda ili kukabiliana na COVID-19. Mwandishi wetu John Kibego anazungumuza na wanafunzi Feza Kabera na Shamil Bao Yahaya ambao wanaeleza jinsi gani wanavyohimili vishawishi vya kupata mimba za utotoni na kujiunga na vikundi vya watumiaji madawa ya kulevya miongoni mwa mengine wakati huu wakiwa majumbani katika kambi ya wakimbizi ya Kyangwali.
Tuitumie COVID-19 kubadili miji yetu:Guterres
atibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres, kupitia ujumbe wake wa uzinduzi wa tamko la kisera kuhusu janga la virusi vya corona katika miji, hii leo ametoa wito kwa viongozi kote duniani kufikiria upya na kurekebisha miji katika kipindi hiki ambacho dunia inapona kutokana na janga la COVID-19 kwani miji imeonekana kuwa kitovu cha janga hilo. Loise Wairimu na taarifa zaidi
(Taarifa ya Loise Wairimu)
Bwana Guterres ameeleza kuwa miji ni kitovu cha COVID-19 kwa kuwa asilimia ya wagonjwa wote wa janga hili wamethibitika kuwa wa mijini.