Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Shule zikiwa zinaanza kufunguliwa, bado hakuna huduma za kujisafi kujikinga na COVID-19- Ripoti
Wakati huu ambapo shule katika maeneo mbalimbali duniani zikihaha kuanza tena mihula mipya baada ya karantini kutokana na janga la virusi vya Corona au COVID-19, ripoti mpya ya mashirika ya Umoja wa Mataifa imeonesha kuwa asilimia 43 ya shule kote ulimwenguni mwaka 2019 hazikuwa na huduma za msingi za kujisafi, ikiwemo kunawa mikono kwa maji safi na sabuni, sharti ambalo ni la msingi kwa shule kuweza kuwa na mazingira salama kwa wanafunzi wakati huu wa janga la COVID-19.
Wagonjwa wa COVID-19 watafikia milioni 20 wiki hii-WHO
Mkurugenzi Mkuu wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa Dkt Tedros Ghebreyesus ameueleza ulimwengu hii leo kuwa, wiki hii idadi ya wagonjwa wa COVID-19 walioathibitishwa itafikia milioni 20 na vifo 750,000 kote duniani kwa hivyo viongozi wanatakiwa kuchukua hatua na raia wanatakiwa kuzifuata au kuzikumbatia hatua mpya.
10 Agosti 2020
COVID-19 imekuwa na athari mbaya kwa zaidi ya watu wa asili milioni 476 kote ulimwenguni.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ujumbe wake kwa njia ya video kuhusu siku ya leo ya watu wa asili ambayo huadhimishwa Agosti 9 ya kila mwaka, amesema ni muhimu kwa nchi kuandaa rasilimali ili kushughulikia mahitaji ya watu wa asili, kuheshimu michango yao na kuheshimu haki zao kujibu mahitaji yao, kuheshimu michango yao na kuheshimu haki zao zisizopingika.
COVID-19 Uganda yawa ‘mwiba’ kwa akina mama wanaonyonyesha watoto
Maziwa ya mama bado hayajathibitishwa kuwa na uwezo wa kuambukiza virusi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto," imesema WHO wakati huu ambapo kuna shaka na shuku kuwa yanaweza kusababisha maambukizi.
Wiki ya kimataifa ya unyonyeshaji mtoto maziwa ya mama ikifikia ukingoni hii leo, shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO, limesema kuwa bado hakuna uthibitisho wowote ya kwamba virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Corona, au COVID-19, vinaweza kuambukizwa kupitia maziwa ya mama.
Mikakati ya kupambana na COVID-19 na kurejea katika hali nzuri, iwahusishe watu wa asili
Dunia ikielekea kuadhimisha siku ya watu wa asili keshokutwa Jumapili Agosti 9, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ujumbe wake kwa njia ya video ameeleza kuwa kuna kila haja ya kutambua haki za watu wa asili na kuwajumuisha katika mapambano dhidi ya COVID-19.
COVID-19 Uganda yawa ‘mwiba’ kwa akina mama wanaonyonyesha watoto
Maziwa ya mama bado hayajathibitishwa kuwa na uwezo wa kuambukiza virusi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto," imesema WHO wakati huu ambapo kuna shaka na shuku kuwa yanaweza kusababisha maambukizi.
WHO kutuma wataalamu wake ili kupambana na COVID-19, Afrika Kusini.
Shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO, kupitia taarifa yake iliyotolewa hii leo mjini Brazzaville, Congo, Geneva Uswisi na Johannesburg Afrika Kusini, limesema linatuma wataalamu wake 43 wenye utaalamu mbalimbali nchini Afrika Kusini ili kusaidia kupambana na ugonjwa wa COVID-19.
Kama maambukizi ya COVID-19 ndani ya jamii yamedhibitiwa, fungueni shule – Guterres
Janga la ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID- 19 likiendelea kuripotiwa maeneo mbalimbali duniani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa tamko lake la kisera lenye lengo la kuhakikisha kuwa janga hilo halizidishi pengo lililokuwa la walio na elimu na wasio na elimu.
Barakoa si tu ni njia ya kujikinga bali pia ni ishara ya mshikamano-WHO
Shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO hii leo Jumatatu limezindua kampeni ya kuhamasisha uvaaji wa barakoa katika kipindi hiki ambacho nchi kadhaa zimeanza kupata nafuu ya COVID-19.