Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

© FAO/Luis Tato

Mfumo wa AFCAFIM unaoratibiwa na IFAD wawezesha wakulima Kenya kuhimili mabadiliko ya tabianchi

Kwa miaka 45, mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Kilimo , IFAD umekuwa ukifadhili wakulima wadogo wadogo na maendeleo vijijini. IFAD inakuwa kama mratibu kwa kushirikiana na benki binafsi na sasa kuna mfumo wa fedha wa kuwezesha wakulima Afrika kukabiliana na kuhimili madhara ya mabadiliko ya tabianchi au ARCAFIM. Mfumo huo umewezesha kupatikana kwa dola milioni 700 za uwekezaji kutoka sekta binafsi kwenye kwa wakulima wadogo huko Kenya, Rwanda, Tanzania na Uganda, ili kutokomeza umaskini na njaa katika maeneo ya vijijini ya nchi zinazoendelea.

Sauti
2'40"
FAO Tanzania

Fahamu jinsi Nukta Fakti ilivyosaidia lishe bora kwa watoto kupitia mtandao

Leo katika makala tunakwenda Tanzania kuzungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya habari na teknolojia ya Nukta Afrika Nuzulack Dausen  ambaye pia mwanzilishi wa Jiko point inayojihusisha zaidi na utoaji habari sahihi kuhusu uhakika wa chakula na lishe, jambo ambalo linapigiwa upatu kila uchao na Umoja wa Mataifa. Amezungumza hivi karibuni jijini Dar es Salaam na Stella Vuzo afisa habari wa Umoja wa Mataifa kufahamu kwa undani wanachokifanya katika kutimiza azma hiyo na anaanza kwa kueleza Jiko point ni nini hasa?

Sauti
3'22"
UN News

Wanazuoni waanza utafiti wa kupunguza maneno ya kigeni katika lugha ya kiswahili

Wakati wadau wa lugha ya kiswahili wakikuna vichwa namna ya kuhakikisha lugha hiyo adhimu inasambaa na kuzungumzwa duniani kote, wengine wanaendelea na utafiti kuhakikisha lugha hiyo inakuwa na maneno ya kiswahili fasaha na kupunguza mchanganyiko wa maneno ya kigeni katika lugha hiyo. 

Leah Mushi aliyehudhuria Kongamano la Kimataifa la Kiswahili lililoandaliwa na Chama cha Ukuzaji wa Kiswahili duniani – CHAUKIDU huko jijini Arusha nchini Tanzania ameketi chini na mwanazuoni huyo na kutuandalia makala haya. 

Sauti
4'36"
Fr. Ayodi/Franciscans.

Ushirikiano wetu ndio siri ya kuwa sehemu ya tuzo hii – Fr. Ayodi

Hii leo kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa kumefanyika hafla la kupatia tuzo washindi wa Tuzo ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu, tuzo inayotolewa kwa mtu mmoja mmoja au kundi kwa kuzingatia mchango wao kwenye kusongesha haki za binadamu. Miongoni mwa washindi wa watano ni Ushirikiano wa kimataifa wa mashirika ya kijamii, watu wa asili, harakati za kijamii na jamii za mashinani. Shirika lisilo la kiserikali la kimataifa la Wafransiskani wakapuchini ni sehemu ya ushirikiano huo.

Sauti
3'48"
Marynsia Mangu

Heko Marynsia kwa ushindi wa tuzo COP28

Marynsia Mangu, mmoja wa washiriki wa COP28 au mkutano wa 28 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Mabadiliko ya Tabianchi, UNFCCC uliofanyika huko Dubai, Falme za Kiarabu, ambaye ameondoka akiwa amebeba tuzo. Tuzo inayodhihirisha utendaji wake yeye kama Afisa Mtendaji Mkuu wa shirika lisilo la kiserikali la Success Hands Tanzania.  Shirika hili linahusika na kuwajengea watoto tabia ya kupenda kusoma vitabu, tena tangu wakiwa tumboni mwa mama zao. Idhaa ya Umoja wa Mataifa ilitaka kufahamu mengi kutoka kwake ikiwemo ni tuzo gani ameshinda.

Sauti
3'58"
© Education Cannot Wait/Daniel Beloumou

Uwekezaji katika elimu kwa watoto utawasaidia kupambana na mabadiliko ya tabianchi

Pazia la mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP28 likitarajiwa kufungwa hapo kesho huko Dubai Falme za kiarabu tunaangazia suala la jinsi mabadiliko ya tabianchi yanavyoathiri watoto hususani katika suala la Afya na kwenye elimu. 

Tarehe 08 Desemba ratiba ya COP28 ilijikita mahususi kujadili masuala ya vijana na watoto. Mashirika mbalimbali yalitoa takwimu zinazohusiana na madhara ya mabadiliko ya tabianchi kwa watoto na vijana moja wao ni Mfuko wa kimataifa wa elimu haiwezi kusubiri ECW. 

Sauti
3'13"
UN News

Kituo cha afya cha Mtofaani kwa hisani ya Milele Zanzibar Foundation utekelezaji wa SDG 3

Shirika lisilo la kiserikali la Milele Zanzibar Foundation la Zanzibar Tanzania ambalo limejipambanua kujikita na utekelezaji wa malengo 12 kati ya malengo 17 ya Umoja wa Mataifa ya Maendeleo Endelevu, limetekeleza lengo namba 3 la Afya Bora na Ustawi kwa kujenga kituo cha afya katika Shehia ya Michikichini, Unguja. Hamad Rashid wa redio washirika wetu Mviwata FM ya Morogoro - Tanzania amefika visiwani humo na kutuandalia makala hii.

Sauti
4'25"
UN News

Siku ya ulemavu duniani: Kauli kutoka kwa mchezesha muziki mwenye ulemavu wa kutoona

Siku ya watu wenye ulemavu duniani iliadhimishwa jana desemba 3 ikiwa na maudhui Ushirikiano katika hatua ya kuokoa na kufikia Malengo ya Maendeleo Endelevu, (SDGs) kwa  pamoja na watu wenye ulemavu, na leo inakupeleka nchini Kenya kummulika mchezeshaji muziki au DJ mwenye ulemavu wa kutoona John Ndichu al maarufu, DJ NdichiKings. Pamela Awuori wa Idhaa hii ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa amezungumza naye akiwa eneo la Ruiru, Kaunti ya Kiambu. 

Sauti
3'14"
UNAIDS

SHDEPHA+ yatekeleza kwa vitendo kauli ya UNAIDS ya jamii zishike hatamu kutokomeza Ukimwi

Leo ni siku ya Ukimwi duniani takwimu zikionesha kupungua sio tu kwa asilimia 70 ya vifo ikilinganishwa na mwaka 2004, idadi ilipokuwa kiwango cha juu zaidi duniani, bali pia maambukizi mapya ikilinganishwa na miaka ya 1980. Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la UNAIDS linasema miongoni mwa sababu za kupungua ni ushiriki wa jamii, yaani jamii kushika hatamu za vita dhidi ya Ukimwi.

Sauti
5'22"
UN News/ Assumpta Massoi

Simulizi: Jina langu ni Selemani lakini nilikuwa naitwa Selina

Wakati kila kona ya dunia kwa sasa ikiadhimisha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia, harakati hizo miaka ya 1987 hazikuwa rahisi kueleweka ndani ya baadhi ya jamii kwani mila na destuli ambazo nyingine zilijikita katika mfumo dume ndizo zilizokuwa zimetamalaki. Lakini wanaharakati walitumia mbinu mbalimbali hata kubadili majina ili waweze kufanya kazi ya kubadilisha mitazamo ndani ya jamii.

Sauti
3'18"