Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

SHDEPHA+ yatekeleza kwa vitendo kauli ya UNAIDS ya jamii zishike hatamu kutokomeza Ukimwi

SHDEPHA+ yatekeleza kwa vitendo kauli ya UNAIDS ya jamii zishike hatamu kutokomeza Ukimwi

Pakua

Leo ni siku ya Ukimwi duniani takwimu zikionesha kupungua sio tu kwa asilimia 70 ya vifo ikilinganishwa na mwaka 2004, idadi ilipokuwa kiwango cha juu zaidi duniani, bali pia maambukizi mapya ikilinganishwa na miaka ya 1980. Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la UNAIDS linasema miongoni mwa sababu za kupungua ni ushiriki wa jamii, yaani jamii kushika hatamu za vita dhidi ya Ukimwi. Hilo ni dhahiri huko nchini Tanzania ambako mashirika ya kiraia ikiwemo mtandao wa kitaifa wa maendeleo ya afya, huduma na uegemezi wa watu waishio na Virusi Vya Ukimwi na Ukimwi, SHDEPHA+, unatekeleza kwa vitendo ujumbe wa mwaka huu wa siku ya Ukimwi duniani, wa Achia Jamii Ziongoze Harakati dhidi ya Ukimwi. Assumpta Massoi anafafanua kinagaubaga kwenye makala hii kile kinachofanyika. 

Audio Credit
Evarist Mapesa/Assumpta Massoi
Sauti
5'22"
Photo Credit
UNAIDS