Wakazi wa Ituri, DRC, wazungumzia usaidizi wa MONUSCO kwenye eneo lao
Katika jimbo la Ituri, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, watu waliokimbia makazi yao wanaishi katika takribani kambi 38, ambapo miongoni mwao ni Drodro, Roe, Lodha, Jaiba na Gina. Zaidi ya wakimbizi Laki Nne (400,000) wanafaidika na ulinzi wa moja kwa moja wa ujumbe wa walinda amani wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO. Walinda amani hao wakiwemo wale wa kutoka Nepal hulinda kambi za watu waliohamishwa kwa kufanya doria za usiku na mchana.