Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

UN News

Wakazi wa Ituri, DRC, wazungumzia usaidizi wa MONUSCO kwenye eneo lao

Katika jimbo la Ituri, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, watu waliokimbia makazi yao wanaishi katika takribani kambi 38, ambapo miongoni mwao ni Drodro, Roe, Lodha, Jaiba na Gina. Zaidi ya wakimbizi Laki Nne (400,000) wanafaidika na ulinzi wa moja kwa moja wa ujumbe wa walinda amani wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO.  Walinda amani hao wakiwemo wale wa kutoka Nepal hulinda kambi za watu waliohamishwa kwa kufanya doria za usiku na mchana.

Sauti
4'24"
IMF/Esther Ruth Mbabazi

EmpowerU Cash+; yabadilisha maisha katika Wilaya ya Lamwo nchini Uganda

Kutokana na ushirikiano kati ya serikali ya Uganda na ya Uholanzi, Mradi wa Maendeleo wa Kukabiliana na Athari za Ufurushwaji (DRDIP), Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) kwa kutumia mfumo wa fedha taslimu wa EmpowerU Cash+.limewasaidia walengwa waliochaguliwa katika Wilaya ya Lamwo ambapo mpango uliwalenga wakimbizi na jamii zilizowapokea.  

Sauti
4'45"
© UNICEF Burundi

Mbinu 3 za kuhakikisha watoto wanapata chanjo

Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya watoto ulimwenguni UNICEF linatumia njia mbalimbali kuhakikisha watoto na familia zao wanapata chanjo stahili hili kuwaepusha kuugua magonjwa ambayo mengine yanaweza kuzuilika kwa kupata chango. Katika Makala hii Leah Mushi anatujuza mbinu tatu zinazotumiwa na UNICEF kuhakikisha jamii inapata chanjo. 

Sauti
3'8"
UNHCR Video

Olga muathirika wa vita Ukraine anasema bila UNHCR sijui ningekaa wapi

Kutana na Olga mwathirika wa vita inayoendelea nchini Ukraine ambaye baada ya nyumba yake kushambuliwa na kombora mjini Borodyanka alikataa tamaa ya Maisha lakini sasa mradi wa UNHCR wa kukarabati nyumba zilizoharibiwa na vita Ukraine umemfufulia matumaini ya Maisha yeye na mwanaye.  Kwa undani zaidi ungana na Flora Nducha kwa makala hii.

Sauti
3'9"
MINUSCA

MINUSCA yachukua hatua kukabili habari potofu n aza uongo CAR

Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR kwa muda mrefu imegubikwa na mizozo ya wenyewe kwa wenyewe hususuan maeneo ya kaskazini mwa nchi. Umoja wa Mataifa umekuwa na juhudi mbalimbali za kuleta amani hadi kuwezesha kufanyika kwa uchaguzi mwaka 2016 uliomwezesha Rais wa sasa Faustin Archange Touadera kuwa madarakani. Ingawa hivyo kumekuweko na changamoto za mivutano huku kuenea kwa habari potofu na za uongo kuwa moja ya kichocheo. Kwa kutambua hilo ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MINUSCA umechukua hatua. Je ni zipi hizo? Ungana na Assumpta Massoi kwenye makala hii. 

Sauti
3'56"
IFAD

Mradi wa IFAD umenisaidia baada ya kuathiriwa na mabadiliko ya tabianchi – Mkulima Kenya

Mradi wa kilimo endelevu unaofadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Kilimo, IFAD na Serikali ya Kenya ambao unalenga kukuza miche ya miti na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi umeleta manufaa kwa wakulima wadogo kutoka eneo la Kaunti ya Kiambu nchini Kenya na kuboresha ukulima wao. Mkulima mdogo Francis Njoroge ni mmoja wa mamilioni ya wakulima wadogo wanaokabiliwa na athari za mabadiliko ya tabianchi lakini kwa bahati nzuri, amefaidika na Mfuko wa Upper Tana Nairobi Water Fund unaolenga kukuza miche ya miti na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Sauti
4'4"
UN News

Kipaji cha sarakasi chamwezesha mkimbizi kutoka DRC kupata elimu bora Uganda

Umoja wa Mataifa unapazia sauti suala la vijana kutumia vipaji vyao ili kuweza kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu .SDGs. Mmoja wa walioitikia wito huo ni mkimbizi kutoka mjini Bukavu jimboni Kivu Kusini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambaye baada ya kuwasili ukimbizini nchini Uganda, kipaji chake cha kucheza sarakasi kimemwezesha kupata elimu bora na hivyo kuwa na uhakika wa ustawi wake na familia yake. Ni kwa vipi kipaji hicho kimemsaidia? John Kibego wa Redio washirika Kazi Njema FM iliyoko Hoima nchini Uganda amezungumza na kijana huyo. 
 

Sauti
4'7"
© FAO/Luis Tato

Mfumo wa AFCAFIM unaoratibiwa na IFAD wawezesha wakulima Kenya kuhimili mabadiliko ya tabianchi

Kwa miaka 45, mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Kilimo , IFAD umekuwa ukifadhili wakulima wadogo wadogo na maendeleo vijijini. IFAD inakuwa kama mratibu kwa kushirikiana na benki binafsi na sasa kuna mfumo wa fedha wa kuwezesha wakulima Afrika kukabiliana na kuhimili madhara ya mabadiliko ya tabianchi au ARCAFIM. Mfumo huo umewezesha kupatikana kwa dola milioni 700 za uwekezaji kutoka sekta binafsi kwenye kwa wakulima wadogo huko Kenya, Rwanda, Tanzania na Uganda, ili kutokomeza umaskini na njaa katika maeneo ya vijijini ya nchi zinazoendelea.

Sauti
2'40"