Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Simulizi: Jina langu ni Selemani lakini nilikuwa naitwa Selina

Simulizi: Jina langu ni Selemani lakini nilikuwa naitwa Selina

Pakua

Wakati kila kona ya dunia kwa sasa ikiadhimisha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia, harakati hizo miaka ya 1987 hazikuwa rahisi kueleweka ndani ya baadhi ya jamii kwani mila na destuli ambazo nyingine zilijikita katika mfumo dume ndizo zilizokuwa zimetamalaki. Lakini wanaharakati walitumia mbinu mbalimbali hata kubadili majina ili waweze kufanya kazi ya kubadilisha mitazamo ndani ya jamii. Mwandishi wa habari nguli Selemani Mkufya kutoka nchini Tanzania anatusimulia alivyofanya kazi na chama cha waandishi wa habari wanawake -TAMWA ambapo huko alikuwa akiitwa Selina badala ya Selemani. 

 

Audio Credit
Assumpta Massoi/Selemani Mkufya
Audio Duration
3'18"
Photo Credit
UN News/ Assumpta Massoi