Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Maji ya kisima hiki ni jawabu kwa afya na kipato – Mwananchi Sudan Kusini

Maji ya kisima hiki ni jawabu kwa afya na kipato – Mwananchi Sudan Kusini

Pakua

Kwa siku tatu, viongozi wakuu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa, lile la Mpango wa Chakula (WFP), Chakula na Kilimo (FAO) na Mfuko wa Maendeleo ya Kilimo duniani, IFAD walikuwemo nchini Sudan Kusini kuona ni kwa jinsi gani miradi wanayotekeleza kwa pamoja ya kujenga mnepo na kuhakikisha lishe ya uhakika na bora imeleta mabadiliko. Wakazi wa Apada Boma jimboni Bahr el Ghazal Kaskazini nchini humo walikuwa taswira ya manufaa ya miradi hiyo ambayo wakuu hao walikagua kama inavyofafanua Makala hii iliyoandaliwa na Assumpta Massoi. 

Audio Credit
Selina Jerobon/Assumpta Massoi
Audio Duration
4'18"
Photo Credit
©FAO/IFAD/WFP/Eduardo Soteras.