Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Sauti za asasi za kiraia katika utekelezaji wa SDGs ni muhimu: UNA

Sauti za asasi za kiraia katika utekelezaji wa SDGs ni muhimu: UNA

Pakua

Jukwaa la ngazi ya juu la kisiasa la Umoja wa Mataifa kuhusu malengo ya maendeleo endelevu HLPF, linaendelea hapa Makao Makuu jijini New York Marekani likitathimini utekelezaji wa malengo hayo yaliyosaliza chini ya miaka 7, kabla ya kufikia ukomo hapo mwaka 2030. Mbali ya tathimini ya utekelezaji wake jukwaa hilo limetoa fursa kwa nchi 39 zilizojitolea kuwasilisha ripoti za kitaifa za utekelezaji wa malengo hayo. Tanzania ni miongoni mwa nchi hizo na iliwasilisha ripoti yake jana Jumanne. Reynald Maeda, Mkurugenzi wa asasi ya Umoja wa Mataifa Tanzania, UNA ni miongoni mwa waliochangia katika ripoti hiyo kwa sasa yuko hapa New York akishiriki jukwaa hilo lakini kabla hajaondoka Tanzania alizungumza na Stella Vuzo wa kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa UNIC Dar es salaam akianza kwa kumueleza mchango wa asasi hiyo katika ripoti iliyowasilishwa.

Audio Credit
Anold Kayanda/Stella Vuzo
Audio Duration
3'52"
Photo Credit
Stella Vuzo/UNIC Dar es