Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Je unafahamu kuwa kuna fursa ya ufadhili katika nishati safi na salama Tanzania?

Je unafahamu kuwa kuna fursa ya ufadhili katika nishati safi na salama Tanzania?

Pakua

Kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la mfuko wa maendeleo ya mitaji UNCDF wakizingatia Utafiti wa Bajeti ya Kaya Tanzania Bara (2017/18), upatikanaji wa nishati safi na teknolojia ya kupikia ni asilimia 17.1 tu ya wakazi wa mijini na asilimia 2 ya wakazi wa vijijini. Kuongezeka kwa mahitaji ya nishati ya kuni kunatokana na ukuaji wa haraka wa miji, bei ya juu, na upatikanaji mdogo wa nishati mbadala. Ili kuondokana na changamoto hizi, Programu ya CookFund ambayo inatekelezwa chini ya UNCDF kwa kushirikiana na Wizara ya Nishati nchini Tanzania, ina nia kuongeza idadi ya watu kwa kutumia suluhu endelevu za nishati safi ya kupikia katika maeneo ya mijini. Tayari awamu ya kwanza ya ufadhili imeenda kwa makampuni 16 kama anavyosimulia Anold Kayanda katika makala hii.
 

Audio Credit
Assumpta Massoi/ Anold Kayanda
Audio Duration
5'22"
Photo Credit
UNDP Zimbabwe