Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kutoka Dodoma Tanzania Bara hadi Paje, Zanzibar kukabiliana na  umaskini

Kutoka Dodoma Tanzania Bara hadi Paje, Zanzibar kukabiliana na  umaskini

Pakua

Moja ya malengo ya Umoja wa Mataifa kuhusu maendeleo endelevu, SDGs ni kutokomeza umaskini ifikapo mwaka 2030. Ikiwa imesalia miaka 7 kabla ya kufikia ukomo, nchi, jamii na kila mtu mmoja mmoja anachukua hatua kutokomeza umaskini hasa kuanzia ngazi ya familia. Umaskini unasababisha watu washindwe sio tu kupata mlo bali pia kupeleka watoto wao shuleni kupata elimu bora. Nchini Tanzania,  hususan visiwani Zanzibar katika mkoa wa Kusini Unguja Assumpta Massoi katika pita ya hapa na pale alikutana na mwananchi mmoja ambaye ameamua kuvuka baharí ya Hindi kutoka Bara  hadi visiwani kukabiliana na umaskini. Ungana naye basi Assumpta Massoi katika makala hii. 

Audio Credit
Selina Jerobon/Assumpta Massoi
Audio Duration
3'36"
Photo Credit
Credit: UN/Assumpta Massoi