UNDP yapiga jeki juhudi za wakulima wa pilipili Tanzania
Nchini Tanzania harakati za kuondokana na umaskini zinaendelea kushika kasi mashinani zikipigiwa chepuo na Umoja wa Mataifa. Miongoni mwa hatua hizo ni kilimo cha kisasa cha mboga mboga na matunda kinachoendeshwa na wanawake kupitia chama cha wakulima wa mboga na matunda nchini Tanzania, TAHA. TAHA imepatiwa msaada na shirika la mpango wa maendeleo la Umoja wa Mataifa UNDP nchini Tanzania na sasa kupitia vikundi mbalimbali, wakulima wanalima mazao ambayo yanakidhi vigezo vya kuuzwa nje ya nchi.