Watoto wa kike Morogoro Tanzania wameitaka jamii kuacha vitendo vya kikatili dhidi yao
Dunia ikiwa katika mfululizo wa siku 16 za kuahamasisha mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia, nchini Tanzania mkoani Morogoro wasichana wamepaza sauti wakionesha kutofurahishwa na ukatili unaofanywa na baadhi ya wazazi na walezi majumbani. Huku wakiiomba serikali kufuata sheria pale mtuhumiwa anapo kamatwa na kufikishwa mahakamani, kwa makosa ya ukatili dhidi ya watoto wa kike.