Tunapowalinda wanyama, tunajilinda wenyewe-Jim Justus Nyamu
Wanyamapori wamekuwa ni kitenga uchumi kwa nchi nyingi za Afrika lakini sekta hii inakumbwa na changamoto za kila siku zikiwemo uwindaji haramu wa wanyama pori wakati ndovu wakiwa miongoni mwa wanyama wanaowindwa zaidi kutokana na thamani ya pembe zake.
Jim Justus Nyamu kutoka nchini Kenya, mwaka 2012 alinzisha kampeni ya kuhamasisha kuhusu umuhimu wa kuwalinda ndovu mwaka 2012, na amefanya ziara katika nchi mbalimbali duniani kufanya shughuli hiyo.
Mwandishi wetu wa Kenya Jason Nyakundi amezungumza na Bwana Nyamu.