Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

UNIC/Stella Vuzo

Mbinu dhidi ya virusi vya Corona zachangia uhifadhi wa mazingira- UNEP

Naam na sasa tuelekee nchini Tanzania kusikiliza sehemu ya mchango au ushiriki wa shirika la mazingira la Umoja wa Mataifa UNEP katika mapambano dhidi ya virusi vya corona, COVID-19. Katika mahojiano haya yaliyofanywa na Hilda Phoya wa kituo cha habari za Umoja wa Mataifa UNIC Dar es salaam, Clara Makenya ambaye ni Mwakilishi wa UNEP nchini Tanzania anaanza kwa kueleza hatua zinazochukuliwa na shirika lake katika kupambana na COVID-19.

 

Mahojiano haya yameandaliwa na Hilda Phoya, UNIC Dar es salaam

 

Sauti
5'39"
WFP/Marco Frattini

COVID-19 yazidisha mzigo  kwa wanawake kusimamia familia Uganda

Mlipuko wa virusi vya corona vinavyosababisha ugonjwa wa COVID-19 umeweka wazi mambo mengi ambayo yanaendelea katika jamii. Mifumo ya kiafya ya nchi mbalimbali, usawa wa kijinsia, uchumi na hata uwezo wa kukabiliana na majanga.  Nchini Uganda hususani maeneo ya magharibi na katikati mwa nchi licha ya wanawake kuwa na jukumu muhimu la kuhudumia familia hususani katika suala la chakula, lakini mtazamo wa jamii juu ya wanawake unawabana katika masuala kadhaa ambayo yamenasibishwa na uanaume zaidi.

Sauti
3'50"
UNDP Moldova

Tunahimiza watu wengi zaidi kuwekeza katika nyuki ili kulinda mazingira na nyuki wenyewe   

Kila tarehe 20 ya mwezi Mei ulimwengu unaazimisha siku ya nyuki duniani ili kukuza uelewa kuhusu umuhimu wa wadudu hawa ambao wanasaidia katika ustawi wa dunia.  Hata hivyo kutokana na shughuli za binadamu, nyuki wanazidi kuwa hatarini japokuwa ni wazi kuwa mchango wao katika uchafushaji wa mimea ni muhimu kwa mstakabali wa ustawi na uwepo wa dunia. Katika kuliona hilo, vijana mkoani Mwanza nchini Tanzania wameanzisha karakana ya kutengeneza mizinga ya kisasa ili kuwanusuru wadudu hao muhimu ikiwa ni pamoja na kujipatia faida nyingine kama asali na kipato.

Sauti
3'23"
FAO Tanzania

Mafunzo ya FAO sasa yamewezesha hata waume zetu kufurahia kilimo- Paskazia

Mashirika ya Umoja wa Mataifa yameendelea kubadilisha maisha ya wananchi kupitia miradi mbalimbali inayotekeleza huko nchini Tanzania.

Miradi hiyo ni pamoja na ule wa kupatia wakulima mbinu bora za kilimo ili kuongeza kipato, kulinda mazingira, kuepusha ukosefu wa chakula na  kutokomeza umaskini, mradi ambao unatekelezwa na FAO ambalo ni shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa, kupitia mradi wa pamoja wa wa Umoja wa Mataifa kwa Kigoma. 

Sauti
4'22"
World Bank/Sambrian Mbaabu

Wahenga walinena ya kale ni dhahabu: Muuguzi Anita Nthumbi

Wakati huu dunia inapopambana na janga la virusi vya corona au  COVID-19 nchi kadhaa zimekumbwa na uhaba wa wataalamu wa afya hasa kwa kuzingatia kwamba idadi ya wagonjwa ni kubwa kuliko uwezo lakini pia katika baadhi ya nchi wahudumu wa afya ni miongoni mwa wagonjwa wa COVID-19. Nchini Kenya hatua mbalimbali zinachukuliwa kushughulikia tatizo la uhavba wa wauguzi katika wakati huu ikiwemo kuwahamasisha wahudumu wa afya wa zamani kurejea kzini ili kusaidia.

Sauti
4'25"
UN

Mvumbuzi kijana atengeneza kifaa cha kuzuia matumizi ya simu yasiyoruhusiwa shuleni

Lengo namba 9 la maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa, SDGs ifikapo 2030 Iinahimiza  juu ya uwepo wa miundombinu bora,viwanda endelevu  na uvumbuzi. Katika kuhakikisha lengo hili linatekelezeka,kijana Boris Maximilian Masesa wa nchini Tanzania amevumbua kifaa maalum kinachoweza kunasa mawasiliano ya simu kwa ajili ya kuwasaidia walimu kuwabaini wanafunzi wanaotumia simu bila ruhusa. Ifuatayo ni makala iliyoandaliwa na  Nyota Simba na kusimuliwa na Evarist Mapesa kutoka Redio washirika SAUT FM iliyopo jijini Mwanza Tanzania.

Sauti
3'49"