Kala Jeremiah anayesifika kwa nyimbo za kijamii, sasa aja na CORONA IPO.
Wakati mapambano dhidi ya virusi vya corona yakiendelea duniani kote, wito umekuwa ukitolewa na shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO kuwa ni jukumu la kila mtu kuwalinda wengine kama anavyojilinda hiyo ikiwa ni pamoja na kusambaza elimu ya kutosha kwa jamii kuhusu namna bora za kujilinda ambazo zinahamasishwa na shirika hilo.