Dr wa hospitali inayoungwa mkono na UM DR Congo apata tuzo
Dr Denis Mukwege, mkuu wa hospitali ya Panzi mjini Bukavu iliyoko Kivu ya Kusini Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ametunukiwa tuzo ya kiamataifa na ufalme wa Ubelgiji mwezi Mai mwaka huu kwa mchango wake katika jamii.
Tuzo hiyo ya kimataifa ambayo hutolewa kila baada ya miaka miwili humuendea mtu ambaye amechangia kwa kila hali kuendeleza maendeleo duniani.