DRC: MONUSCO yafunga rasmi virago Kivu Kusini, yasalia Ituri na Kivu Kaskazini
Operesheni za kijeshi za ulinzi wa amani zilizokuwa zinafanywa na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC huko jimboni Kivu Kusini zimekamilika Jumanne ya Aprili 30, 2024 kwa mujibu wa azimio namba 2717 la mwezi Desemba 2023, la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.