Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Kampuni ya Yvette Amuli, (pichani) iitwayo Kiyana ni miongoni mwa wanufaika wa mradi wa kampuni ndogo na za kati, SME's unaoendeshwa kwa pamoja kati ya Benki ya Dunia na UN Women kwa ushirikiano na Sowers of New Hope, huko Goma, mji mkuu wa jimbo la Kivu…
UN/ Byobe Malenga

Asilimia 40 ya nchi za kipato cha chini zitakuwa maskini zaidi kuliko kabla ya COVID-19

Benki ya Dunia kupitia ripoti ya matarajio ya uchumi kwa mwaka huu wa 2024 inaeleza kuwa baada ya uchumi wa mwaka 2023 kufanya vibaya, nchi za kipato cha chini zitakua kwa 5.5%, chini ya ilivyotarajiwa na kwamba kufikia mwisho wa 2024, karibu 25% ya nchi zinazoendelea na karibu 40% ya nchi za kipato cha chini zitakuwa maskini kuliko kabla ya janga la COVID-19.

Mhudumu wa afya akifunga bandeji kwenye mguu wa mtoto katika hospitali moja huko Gaza.
© WHO

HABARI KWA UFUPI: Gaza, Ukraine, Uchumi

Kwa mujibu wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa duniani WHO na timu yake iliyoko katika ukanda wa Gaza, idadi ya vifo na majeruhi kutokana na mzozo unaoendelea baina ya Israel na kundi la Hamas inaongezeka kila uchao na waathirika wakubwa ni wanawake na watoto. Akitoa takwimu katika mkutano na waandishi wa habari mjini Geneva Uswis hii leo mwakilishi wa WHO kwenye eneo linalokaliwa la Palestina Dkt. Rik Peeperkorn amesema “Kutokana na takwimu za wizara ya afya ya Gaza tunazungumzia zaidi ya watu 23,000 waliokufa ambapo asilimia 70 ni wanawake na watoto, takriban watu wengine elfu 59 wamejeruhiwa ambao ni asilimia 2.5 ya watu wote, na asilimia 3.5 ya watu wote wameathirika moja kwa moja.”

Francis Njoroge, Mkulima kutoka Muranga nchini Kenya.
IFAD

Mkulima Kenya: Mradi wa IFAD umenisaidia baada ya kuathiriwa na mabadiliko ya tabianchi

Mradi wa kilimo endelevu unaofadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Kilimo, IFAD na Serikali ya Kenya ambao unalenga kukuza miche ya miti na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi umeleta manufaa kwa wakulima wadogo kutoka eneo la Kaunti ya Kiambu nchini Kenya na kuboresha ukulima wao. Mkulima mdogo Francis Njoroge ni mmoja wa mamilioni ya wakulima wadogo wanaokabiliwa na athari za mabadiliko ya tabianchi lakini kwa bahati nzuri, amefaidika na Mfuko wa Upper Tana Nairobi Water Fund unaolenga kukuza miche ya miti na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Sauti
4'4"