Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Watu milioni moja wamelazimika kukimbia katika muda wa wiki tatu zilizopita huku mashambulizi makubwa ya mabomu yakiendelea huko Rafah kusini mwa Gaza.
© UNRWA

Vita Gaza imemong’onyoa utangamano wa kijamii - OCHA

Kadri siku zinavyozidi kusonga na mashambulizi yakiendelea huko Gaza, nafasi iliyosalia kwa ajili ya raia wa Gaza inazidi kuwa finyu huku mazingira ya maisha yakimong’onyoa utangamano wa kijamii amesema Afisa mwandamizi wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya dharura, OCHA kwenye eneo hilo la wapalestina linalokaliwa na Israeli.

Wahamiaji wa Afrika Mashariki waliojaribu kuvuka bahari ya Mediterania wanaokolewa na jeshi la wanamaji la Italia huko Sicily.
© UNICEF/Gideon Mendel

Kuna mapungufu makubwa katika huduma za ulinzi kwenye njia za uhamiaji kutoka Afrika hadi Ulaya: UNHCR

Ukosefu wa huduma za ulinzi katika njia kuu zinazotumiwa na wakimbizi na wahamiaji wakitokea Afrika kuelekea Ulaya ni jambo la kutisha na  limekuwa baya zaidi katika miaka ya hivi karibuni, kulingana na ripoti mpya ya Shirika la Umoja wa mataifa  la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR ambayo inaangazia mahitaji makubwa na hatari wanazokabiliana nazo.

Walinda amani wa Umoja wa Mataifa wanaohudumu kwenye ujumbe wa Umoja huo wa kulinda amani nchini DRC, MONUSCO wakiwa kwenye doria katika kijiji cha Logo mji wa Djugu jimboni Ituri .
MONUSCO

Walinda amani wa UN waweka doria kali mashariki mwa DRC baada ya kuibuka mapigano

Katika kukabiliana na hali ya mapigano makali yaliyoibuka tena mwishoni mwa wiki kati ya kundi lenye kujihami kwa silaha M23 na Jeshi la DR Congo (FARDC), walinda amani wa Umoja wa Mataifa kwa uratibu wa FARDC, wameweka doria karibu na Kanyabayonga kusaidia baadhi ya wanaume, wanawake na watoto 150,000 waliokimbia makazi yao katika siku za hivi karibuni mashariki mwa nchi.

Nyanya ameketi na wajukuu zake watatu waliojeruhiwa kwa mafuriko ya ghafla yalipopiga kijiji chao katika jimbo la Baghlan, Afghanistan.
© UNICEF/Osman Khayyam

Mafuriko ya ghafla Afghanistan ni tishio kubwa kwa watoto: UNICEF

Makumi ya maelfu ya watoto nchini Afghanistan wbado wameathiriwa na mafuriko yanayoendelea, hususan katika majimbo ya kaskazini ya Baghlan na Badakhshan na mkoa wa Ghor magharibi mwa Afghanistan, limesema leo shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia watoto UNICEF na kukumbusha kuwa mafuriko katika nchi hiyo ya Asia ya Kati yanasababisha tishio la haraka na la kudumu kwa watoto.