Vita Gaza imemong’onyoa utangamano wa kijamii - OCHA
Kadri siku zinavyozidi kusonga na mashambulizi yakiendelea huko Gaza, nafasi iliyosalia kwa ajili ya raia wa Gaza inazidi kuwa finyu huku mazingira ya maisha yakimong’onyoa utangamano wa kijamii amesema Afisa mwandamizi wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya dharura, OCHA kwenye eneo hilo la wapalestina linalokaliwa na Israeli.