UNHCR inaendela kupokea na kuandikisha wakimbizi kutoka Ethiopia wanaoingia Sudan
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR linaendelea kuandikisha wakimbizi wapya katika mpaka wa Sudan na Ethiopia ambapo takriban wakimbizi 800 wamevuka kutoka eneo la Tigray nchini Ethiopia na kuingia mashariki mwa Sudan katika siku chache za mwaka huu wa 2021.