UNPOL yaelimisha wanakijiji Darfur masuala ya haki za binadamu
Ikiwa leo ni siku ya haki za binadamu duniani ambayo huadhimishwa kila mwaka Desemba 10, huko Khor Abeche kwenye jimbo la Darfur nchini Sudan, polisi wa Umoja wa Mataifa, UNPOL kwenye ujumbe wa pamoja wa Umoja huo na Muungano wa Afrika (UNAMID) wametamatisha kampeni ya siku 16 ya kupinga ukatili dhidi ya kijinsia kwa kutoa mafunzo ya kusongesha haki za binadamu. Taarifa iliyoandaliwa na Luteni Japhet Chaula, afisa habari wa kikos cha 13 cha Tanzania huko UNAMID inasomwa hapa studio na Grace Kaneiya.