Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

UNAMID kwa kushirikiana na Kamati ya Darfur Kaskazini kuhusu wanawake, iliandaa siku moja majadiliano ya azimio namba 1325 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu wanawake, amani na usalama Darfur Kaskazini
UNAMID/Albert González Farran

UNPOL yaelimisha wanakijiji Darfur masuala ya haki za binadamu 

Ikiwa leo ni siku ya haki za binadamu duniani ambayo huadhimishwa kila mwaka Desemba 10, huko Khor Abeche kwenye jimbo la Darfur nchini Sudan, polisi wa Umoja wa Mataifa, UNPOL kwenye ujumbe wa pamoja wa Umoja huo na Muungano wa Afrika (UNAMID) wametamatisha kampeni ya siku 16 ya kupinga ukatili dhidi ya kijinsia kwa kutoa mafunzo ya kusongesha haki za binadamu. Taarifa iliyoandaliwa na Luteni Japhet Chaula, afisa habari wa kikos cha 13 cha Tanzania huko UNAMID inasomwa hapa studio na Grace Kaneiya. 

Sauti
2'18"
Nakala za awali za tamko la haki za bindamu.
UN Picha/Greg Kinch

Tamko la Haki za Binadamu ni chanjo dhidi ya madhila ya sasa- Bachelet

Inastaajabisha baadhi ya viongozi wa kisiasa wanaendelea kupuuza ugonjwa wa Corona au COVID-19 sambamba na mbinu za rahisi za kujikinga kama kuvaa barakoa na kuepusha mikusanyiko mikubwa. Hiyo ni kauli ya Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu kwenye Umoja wa Mataifa, Michelle Bachelet aliyotoa wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Geneva, Uswisi akitoa ujumbe wake wa siku ya haki za binadamu hii leo, ujumbe ambao umemulika kwa kiasi kikubwa janga la COVID-19 na linavyosigina haki za binadamu.

Moshi kutoka kwa nyumba ya kuoka mikate inayotumia mkaa.
UNICEF/Shehzad Noorani

Kupungua kwa hewa chafuzi angani kunaweza kusaidia kufikia lengo la chini ya nyuzi joto 2 za Selisiasi-UNEP 

Janga la uchafuzi wa hali ya hewa linaweza kupungua hadi asilimia 25 kwenye uzalishaji wa hewa chafuzi uliotabiriwa kufikia mwaka 2030 na hivyo kuileta dunia karibu kufikia lengo la nyuzi joto 2 kipimo cha selisiasi za Mkataba wa Paris, imeeleza ripoti mpya ya shirika la mazingira la Umoja wa Mataifa, UNEP.   

Wakimbizi kutoka Côte d’Ivoire wakisubiri kuandikishwa huko Liberia Oktoba 2020.
© UNHCR/Roland Tuley

Idadi ya watu wanaohama kwa kulazimishwa yavuka milioni 80, COVID-19 nayo ikizidisha machungu

Wakati picha kamili ya mwaka 2020 bado haijafahamika, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR, linakadiria kuwa uhamishaji wa kulazimishwa ulimwenguni au ufurushwaji ulizidi milioni 80 katikati ya mwaka, kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa hii leo mjini Geneva Uswisi kuhusu mwenendo wa uhamishaji wa kulazimishwa ulimwenguni.  

Ukosefu wa uaifa ni changamoto inayowakumba watu wengi.
© UNDP/Mirfozil Khasanov

Ninaishi bila utaifa kwa zaidi ya miongo 7 sasa: Sergio Chakaloff 

Kutana na Sergio Chekaloff ambaye kwa zaidi ya miongo saba anaishi bila utaifa baada ya nchi tatu alizodhani kuwa ni asili yake ambazo ni Ujerumani, Urusi na Armenia zote kukataa kumtambua na  sasa kwa msaada wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR anaishi Ibiza nchini Hispania baada ya kupewa hadhi ya kutokuwa na utaifa. Kulikoni?

Sauti
2'7"