Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mtoto wa Miaka Saba Francesca(sio jina sahihi)akipata matibabu kutoka kwa Daktari Antonella Tonchiaro ktika makazi yasio rasmi anapo ishi Rome nchini Italy.Daktari Tochiaro ni mmoja wa wafanyikazi wa INTERSOS/UNICEF.
© UNICEF/Alessio Romenzi

Miongozo mipya yatolewa kuhusu njia ya ufunguzi salama wa shule hali itakapotengamaa

Mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa lile la elimu, sayansi na utamaduni UNESCO, la kuhudumia watoto UNICEF kwa kushirikiana na Benki ya dunia, hii leo mjini New York Marekani, Paris Ufaransa na Roma Italia, wametoa miongozo kuhusu namna salama ya kuzifungua shule kutokana na kufungwa ambako kunawaathiri takribani wanafunzi bilioni 1.3 kote duniani.

Katibu Mkuu Antonio Guterres akitoa ujumbe kuhusu Janga la COVID-19.
UN Photo/Eskinder Debebe)

Usitishaji uhasama kimataifa, kusaidia wasiojiweza na mikakati ya kujikwamua ndio kipaumbele cha UN:Guterres

 Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres leo Alhamisi ameweka bayana dhimira ya Umoja wa Mataifa ya kutaka kuvishinda vita dhidi ya janga la virusi vya corona au COVID-19  kwa kujikita na mambo matatu muhimu ambayo ni kufikia usitishwaji wa uhasama kimataifa, kuwasaidia wale wasiojiweza na kujiandaa kujikwamua kiuchumi na kijamii kutoka kwenye janga hili.