Moratinos achukizwa na kitendo cha Quran Tukufu kuchomwa moto nchini Sweden
Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya muungano wa ustaarabu, UNAOC Miguel Moratinos amelaani vikali kitendo cha kuchomwa kwa Quran Tukufu kilichofanywa na watu wenye misimamo mikali kwenye mji wa Malmo nchini Sweden.