Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mama huko Mbarara, Uganda Magharibi, anahakikisha kuwa watoto wake wote wanapata dawa ARVs za watoto kwa wakati mmoja kila siku.
© UNICEF/Karin Schermbrucke

Ubia wa UNICEF na serikali Uganda waleta nuru kwa waishio na VVU 

Nchini Uganda, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, kwa kushirikiana na serikali, limechukua hatua kuhakikisha kuwa huduma za msingi za kiafya za kuokoa maisha ikiwemo dawa za kupunguza makali ya UKIMWI zinapatikana hata wakati huu wa vizuizi vya ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19. 

Sauti
2'15"
Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataif kwa Syria, Geir O.pedersen akizungumza na wanahabari. (PIcha ya maktaba)
UN Photo/Evan Schneider

Natiwa moyo na angalau kuwepo kwa misimamo ya pamoja baina ya pande kinzani Syria- Pedersen 

Wajumbe wa pande kinzani nchini Syria wanaokutana mjini Geneva, Uswisi kwa lengo la kusaka suluhu ya kudumu na kumaliza mzozo wa takribani muongo mmoja nchini mwao, angalau wamekuwa na misimamo inayofanana itakayoweza kusongesha mbele majadiliano, amesema Geir Pedersen, Mjumbe Maalum wa Umoja wa Mataifa kwa mzozo wa Syria.