Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Ukosefu wa utaifa ni changamoto
© UNICEF/UNI193657/Esiebo

Usiombe ukutwe na hali ya kukosa utaifa!  

Kutana na Mpho Modise, mama wa watoto wanne ambaye licha ya kuishi nchini Afrika Kusini hana uhakika wa utaifa wake na hivyo anashindwa kupata huduma za msingi kama vile afya na hofu yake kubwa ni kwamba shida inayomkabili yeye ya kukosa utaifa inaweza kuhamia kwa watoto wake labda apate utaifa wa Afrika Kusini.

Sauti
2'21"
Wakimbizi warohingya bado wanaishi wilaya ya Cox's Bazar nchini Bangladesh miaka kadhaa tangu wakimbie nchi yao ya Mynamar
© UNFPA Bangladesh/Carly Learson

WFP imelifungua tena soko la wakulima Cox's Bazar baada ya kulifunga sababu ya COVID-19 

Shirika la mpango wa chakula la Umoja wa Mataifa WFP wiki hii limelifungua  tena soko kubwa la wakulima kwenye kambi ya wakimbizi wa Rohingya ya Cox’s Bazar nchini Bangladesh baada ya kulifunga kwa miezi kadhaa kufuatia mlipuko wa janga la corona au COVID-19. Soko hilo ambalo ni sehemu ya mradi wa WFP ni neema sio tu kwa wakimbizi bali pia jamii inayowahifadhi.

Sauti
2'35"