Mkuu wa UN alaani vikali shambulio la roketi Kabul
Mji mkuu wa Afghanistan, Kabul leo umeshambuliwa kwa roketi na kusababisha vifo na majeruhi kwa raia wengi.
Mji mkuu wa Afghanistan, Kabul leo umeshambuliwa kwa roketi na kusababisha vifo na majeruhi kwa raia wengi.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amezipongeza nchi za ukanda wa Maziwa Makuu barani Afrika kwa hatua kubwa walizofikia hivi karibuni katika kuboresha uhusiano kati ya nchi za Ukanda huo, kupambana na vikundi vyenye silaha na pia maendeleo katika suala la ujumuishaji, kukuza uchumi wa ukanda huo na haki za binadamu.
Katika mkesha wa kuamkia uchaguzi mkuu wa Rais na wabunge nchini Burkina Faso hapo kesho Jumapili Novemba 22, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameipongeza serikali, viongozi wa kisiasa na watu wa Burkina Faso kwa kudumisha mazingira ya kuheshimiana katika wakati wote wa mchakato wa uchaguzi licha ya changamoto lukuki zinazolikabili taifa hilo la Afrika Magharibi.
Siku ya uvuvi duniani huadhimishwa kila mwaka tarehe 21 Novemba kote duniani na hususani jamii za wavuvi.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema anafuatilia kwa karibu hali inayoendelea hivi sasa nchini Uganda na kusema anatiwa hofu na ripoti za machafuko na mauaji kufuatia maandamano yanayofanyika mjini Kampala.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amerkaribisha hatua ya jana Ijumaa ya Muungano wa Afrika AU, ya uteuzi wa wajumbe watatu wa ngazi ya juu ili kusaidia juhudi za kusaka suluhu ya amani ya mgogoro wa jimbo la Tigray nchini Ethiopia.
Maxwell Matewere, mtaalamu katika ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuzuia uhalifu na madawa ya kulevya, (UNODC) nchini Malawi, amekuwa akiendelea na harakati zake za kukabiliana na usafirishaji haramu wa binadamu kwa zaidi ya miongo miwili. Leo hii anapatia mafunzo maafisa mbali mbali nchini Malawi kuzuia na kukabili uhalifu: mwaka huu pekee licha ya janga la Corona au COVID-19, ameweza kuokoa watu 300 waliokuwa wakumbwa na usafirishaji haramu sambamba na kukamata watu 31 wahusika wa uhalifu huo.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akiwahutubia wanahabari hii leo mjini New York Marekani, kuhusu mkutano wa kesho wa viongozi wa nchi 20 zilizo na uchumi mkubwa duniani, G20, ameanza kwa kueleza kuwa mkutano huu unakuja wakati ambao janga la COVID-19 linaendelea kuuharibu ulimwengu.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR limesafirisha kundi la wahamiaji 79 kutoka Libya kwenda Rwanda, ikiwa ni sehemu ya kuhamisha wahamiaji walio hatarini zaidi kwenda maeneo salama.
Shirika la uhamiaji la Umoja wa Mataifa, IOM limeeleza wasiwasi mkubwa juu ya ongezeko la vifo vya wahamiaji vinavyotokea wakati wakisafiri kutoka pwani za Afrika kueleka visiwa vya Canary barani Ulaya.