Kila sekunde 100, mtoto 1 aliambukizwa VVU mwaka jana-UNICEF
Takribani kila dakika moja na sekunde 40, mtoto au kijana chini ya umri wa miaka 20 alikuwa anaambukizwa Virusi Vya UKIMWI, VVU mwaka jana 2019, na kufanya idadi ya watoto wanaoishi na VVU kufikia milioni 2.8, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF limesema katika ripoti yake iliyotolewa leo mjini New York Marekani na Johannesburg Afrika Kusini.