Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mwanamke mwenye VVU anapokea dawa kwa ajili ya mtoto wake wa umri wa siku tatu katika hospitali huko Ouagadougou, Burkina Faso.
UNICEF/Frank Dejongh

Kila sekunde 100, mtoto 1 aliambukizwa VVU mwaka jana-UNICEF 

Takribani kila dakika moja na sekunde 40, mtoto au kijana chini ya umri wa miaka 20 alikuwa anaambukizwa Virusi Vya UKIMWI, VVU mwaka jana 2019, na kufanya idadi ya watoto wanaoishi na VVU kufikia milioni 2.8, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF limesema katika ripoti yake iliyotolewa leo mjini New York Marekani na Johannesburg Afrika Kusini. 

Mwanamke akiwa amembeba binti yake katika kituo cha Wisdom kilichopo eneo la Gurei mjini Juba nchini Sudan kusini baada ya kupigwa na mumewe.
© UNICEF/Albert Gonzalez Farran

UN yaachia dola milioni 25 kwa ajili ya wanawake wanaopambana na unyanyasaji wa kijinsia  

Mkuu ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoshughulikia misaada ya dharura, OCHA, Mark Lowcock hii leo mjini New York Marekani ametangaza kuwa zimetolewa dola za kimarekani milioni 25 kutoka kwenye mfuko wa dharura wa Umoja wa Mataifa, CERF, kusaidia mashirika yanayoongozwa na wanawake ambayo yanapambana dhidi ya unyanyasaji wa kijinsia.

Wanafunzi wa shule ilioko  kijijini Koroko Foumasa Nchini Cote d'Ivoire wakichukua chakula chao cha mchana.
© UNICEF/Frank Dejongh

Rwanda na Cote d’Ivoire miongoni mwa watakaonufaika na msaada wa chakula shuleni-WFP  

Wakati shule katika nchi zinazoendelea, zikianza kufunguliwa, shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula, WFP limepokea msaada wa dola milioni 119 kutoka Idara ya kilimo ya serikali ya Marekani ili kusaidia kutoa chakula katika shule kwenye nchi za Asia na Afrika, imeeleza taarifa ya WFP iliyotolewa hii leo mjini Washington Marekani.