Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Vijana wakulima Lebanon washiriki kupunguza makali ya COVID-19 kwa jamii zao

Familia zilizotawanywa wanahitaji maji, vifaa vya kujisafi ili kuweza kuepukana na COVID-19.
UNICEF Lebanon
Familia zilizotawanywa wanahitaji maji, vifaa vya kujisafi ili kuweza kuepukana na COVID-19.

Vijana wakulima Lebanon washiriki kupunguza makali ya COVID-19 kwa jamii zao

Afya

Nchini Lebanon, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF kwa kushirikiana na shirika  la  kiraia  liitwalo  LOST,  linajumuisha  vijana katika kusaidia watu kukabiliana na athari za ugonjwa unaosababishwa na virusi vya Corona au COVID-19. 

Katika viunga vya mji mkuu wa Lebanon, Beirut, vijana wakiendelea na shughuli za kilimo, na kwingineko  mazao  yaliyovunwa  na vyakula vikiandaliwa kuwafikia walaji.

COVID19 imesababisha baadhi ya watu kushindwa kupata mlo na ndipo UNICEF na LOST wakaingia ubia.  Muasisi wa LOST 

Rammy Lakkis, anaelezeawanavyofanya kazi.“Tuna kundi kubwa la vijana ambao sasa wakokwenye kilimo wakichangia uzalishaji wa chakula nawengine kwenye usindikaji wa vyakula. Pia kunakundi la vijana UNICEF ambao kila siku wanapika  chakula na kukipeleka kama mgao kwa familia.”

Mratibu wa barubaru UNICEF, Amal Obeid anasema  kuwa  mkakati  wao  una  pande  mbili;  Mosi  jinsi  ya kukabili  athari  kwa  jamii zitokanazo na coronavirus">COVID-19 napili kuweka fursa za ajira kwa vijana ili kusaidia kupunguza madhara ya Corona kwa jamii za Lebanon.

Kila siku wanapika mlo kwa takribani watu 500 na mlohuo hufikia wahitaji kwa wakati muafaka tena ukiwawa moto na mpishi wa LOST Ali Saad anasema vijanawanatekeleza jukumu hilo kwa upendo wa dhati.

Kwa vijana washiriki wa mradi huu, limekuwa ni jambo la faraja ambapo Siham Asaf anasema, “ninafurahia  hapa  kwa  sababu  najifunza stadi mpya. Watu wengi wanakufa njaa, watu wengi wanamahitaji mengi! Vyakula na vitamutamutunavyoandaa vinafikia wahitaji.”

Kijana mwingine anasema,“Tunajifunza mambo mengi ambayo awalihatukufahamu. Hivi “

Hatma ya mradi huu ni kuangazia dhima ya vijanakama kichocheo muhimu cha mabadiliko yanayowezakutatua matatizo yanayokumba jamii zao.