Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Watoto wakiwa darasani nchini Sudan Kusini
UNICEF/Shehzad Noorani

Umewahi kusikia kuhusu mwanaharakati wa hisabati? 

Dunia inakuwa mahali bora pa kuishi ikiwa kila mtu atachangia katika kutaka hali hiyo itokee. Kutana na Yusuf Adamu Ibrahim, mwanaharakati mchanga wa hisabati kutoka jimbo la Bauchi, Nigeria ambaye anabadilisha maisha ya watoto wa shule katika jamii yake kwa kuwasaidia kuboresha ujuzi wao wa hesabu. Yusuf ni hamasa kwa wengi, na ni kijana mdogo wa umri wa miaka 18 mpenda mabadiliko.

Sauti
2'21"
Mwanamke aliyefurushwa akiwa ndani ya hema kwenye kambi ya muda, Gao inayohifadhi familia 300 waliokimbia makwao Tessit, Mali kufuatia mzozo.
© UNOCHA/Michele Cattani

COVID-19 yazidisha makadirio ya mahitaji ya kibinadamu 2021 

Watu milioni 235 duniani kote watahitaji misaada ya kibinadamu na ulinzi mwakani 2021, ikiwa ni idadi kubwa zaidi kuwahi kufikiwa, amesema mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa inayohusika na uratibu wa misaada ya kibinadamu (OCHA) Mark Lowcock hii leo, akitaja fedha zinazohitajika kukidhi operesheni hizo kuwa ni dola bilioni 35.