Mkutano wa kwanza wa uchumi na wanyamapori Afrika wafanyika Zimbabwe:UNEP
Wakuu wanne wa nchi wamekutana katika mkutano wa kwanza kabisa kuwahi kufanyika Afrika kuhusu uchumi na masuala ya wanyamapori.
Wakuu wanne wa nchi wamekutana katika mkutano wa kwanza kabisa kuwahi kufanyika Afrika kuhusu uchumi na masuala ya wanyamapori.
Umri wa mwanamke kuolewa umeongezeka duniani kote na viwango vya uzazi vimeshuka huku wanawake wakizidi kuwa na nguvu kiuchumi, imesema ripoti mpya iliyotolewa leo na Umoja wa Mataifa kuhusu mienendo ya maendeleo ya wanawake duniani bila kusahau familia.
Umoja wa Mataifa umeisihi dunia kushikamana na wakimbizi ambao wamelazimika kufungasha virago kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo vita, mauaji , njaa na hata mateso kwani wanachokitaka ni amani.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo limekutana kujadili ya kisiasa na kibinadamu nchini Yemen ambapo mjumbe maalum wa umoja huo kwa Yemen Martin Griffiths amesema ghasia kwenye majimbo sita nchini humo zimepungua kufuatia pande husika kwenye mkataba wa Hudaydah kupunguza mapigano licha ya kwamba utekelezaji wa mkataba huo haujawa kikamilifu.
Lazarus Chigwandali, mmoja wa watu wenye ualibino kutoka Malawi ambaye sasa anatumia kipaji chake cha ameomba kuwepo kwa mfuko wa kujengea uwezo watu wenye ulemavu wa ngozi barani Afrika ili waweze kushiriki kwenye shughuli za kiuchumi na hatimaye kujiongezea kipato na kujikwamua kimaisha. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.
Afrika imepiga hatua japo kiasi katika zama za kidijitali hasa masuala ya teknolojia ya mitandao ingawa safari bado ni ndefu.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres leo amepokea ripoti ya jopo la ngazi ya juu alilounda kuhusu masuala ya ushirikiano wa kidijitali, ripoti ambayo amekabidhiwa na wenyeviti wenza wa jopo hilo Melinda Gates wa taasisi ya Bill and Melinda Gates na Jack Ma ambaye ni Mwenyekiti Mtendaji wa kundi la Alibaba.
Kuelekea maadhimisho ya kwanza kabisa duniani ya siku ya kimataifa ya chakula kesho Juni 7, shirika la afya ulimwenguni, WHO limetaka kuimarishwa zaidi kwa juhudi za kuhakikisha kuwa chakula ambacho kinaliwa ni salama.
Duniani kote kuanzia kwenye miji mikubwa hadi midogo kila mtu anavuta hewa chafu, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kwenye ujumbe wake wa siku ya mazingira duniani inayoadhimishwa tarehe 5 mwezi Juni kila mwaka ikiwa na maudhui tokomeza uchafuzi wa hewa.
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, leo limemchagua mwanadiplomasia na mwanazuoni kutoka Nigeria Tijjani Mohammad Bande kuwa rais wa mkutano wa 74 wa baraza hilo utakaoanza mwezi Septemba mwaka huu hadi Septemba mwakani.