Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mwananchi wa Yemen akisukuma mkokoteni wenye chakula cha msaada huko kwenye mji mkuu Sana'a. Mapigano yamesababisha raia wengi kutegemea chakula cha msaada (3 February 3019)
WFP/Annabel Symington

Ghasia angalau zimepungua kidogo Yemen- Griffths

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo limekutana kujadili ya kisiasa na kibinadamu nchini Yemen ambapo mjumbe maalum wa umoja huo kwa Yemen Martin Griffiths amesema ghasia kwenye majimbo sita nchini humo zimepungua kufuatia pande husika kwenye mkataba wa Hudaydah kupunguza mapigano licha ya kwamba utekelezaji wa mkataba huo haujawa kikamilifu.