Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tuhuma za matumizi ya silaha za kikemikali zijibiwe vilivyo

Izumi Nakamistu mwakilishi wa ngazi ya juu katika idara ya upokonyaji silaha ya Umoja wa Mataifa.(Picha:UM/Manuel Elias)

Tuhuma za matumizi ya silaha za kikemikali zijibiwe vilivyo

Amani na Usalama

Mwakilishi wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa  kuhusu masuala ya upokonyaji silaha Izumi Nakamitsu amesema ushahidi zaidi  wa matumizi wa silaha za  sumu zilizopigwa marufuku nchini Syria ni sharti zipewe jibu la kutosha na Baraza la Usalama la umoja huo.

Bi. Nakamitsu amesema hayo leo wakati akihutubia Baraza la Usalama kuhusu kazi inayofanywa na Umoja wa Mataifa pamoja na a shirika la pamoja la kupinga matumizi ya silaha za kemikali. 

Amesema kuwa uteketezwaji kamili wa vituo  vya serikali 27 unapashwa kukamilishwa katika kipindi kijacho cha miezi miwili na kuongeza kuwa kikosi cha OPCW kinachotafuta ukweli -FFM- katika madai ya  vikosi vya serikali kutumia silaha za sumu kitawasilisha ripoti yake haraka iwezekanavyo.

Madai mengi yanahusu matumizi ya gesi ya Chlorine. Madai hayo baado yanasikika ikiwemo matumizi yake mwishoni mwa juma lililopita katika mji wa Saraqed.

Taarifa zasema kuwa watu tisa wamehudumiwa wakiwa na matatizo ya kupumua baada ya shambulio la bomu linalodhaniwa lilikuwa na gesi katika eneo la mji wa Idlib linalodhibitiwa na waasi.