Benjamin William Mkapa alikuwa mwanadiplomasia mmbobevu na mpenda amani- Guterres
Kufuatia kifo cha Rais wa zamani wa Tanzania Benjamin William Mkapa, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema hayati Mkapa alikuwa mwanadiplomasia mbobevu na mpigania amani anayeheshimika ambaye alihamasisha maridhiano.