Zaidi ya wahudumu wa kibinadamu 140 waliuawa mwaka jana, wengi wao wa kitaifa
Kuelekea siku ya usaidizi wa kibinadamu duniani tarehe 19 mwezi huu wa Agosti, Umoja wa Mataifa leo umesema kadri majanga yanavyozidi kuongezeka duniani maisha ya watoa misaada yako hatarini zaidi na kwamba mwaka jana pekee wa 2021 wahudumu zaidi ya 140 wa kiutu waliuawa duniani kote.