Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Somalia

Familia za Wasomali zilikimbia makazi yao huko Dhobley karibu na mpaka wa Somalia na Kenya.
FAO Somalia

Tusisubiri baa la njaa litangazwe ndio tuisaidie Somalia: FAO

Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO nchini Somalia limetoa ombi la dola milioni 131.4 ili kusaidia wananchi 882,000 kutoka wilaya 55 wenye uhitaji wa haraka wa msaada wa kuokoa maisha yao. FAO wameisihi jumuiya ya kimataifa kutosubiri mpaka nchi hiyo itangaze kuwa na baa la ndio hatua zichukuliwe na badala yake wameomba hatua kuchukuliwa sasa.

Sauti
3'1"
Watoto wakimbizi wa ndani huko Ituri nchini DRC.
UN/Eskinder Debebe

Mauaji na utekaji nyara wa watoto kwenye maeneo ya vita vilishamiri mwaka 2021- Ripoti

Mwaka wa 2021  umeshuhudia mchanganyiko wa mwendelezo hatari wa mizozo, mapinduzi ya kijeshi sambamba na mizozo mipya na ile iliyodumu muda mrefu na ukiukwaji mkubwa wa sheria za kimataifa, vyote ambavyo kwa pamoja vimekuwa na madhara makubwa kwa watoto duniani kote, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ripoti yake ya mwaka kuhusu Watoto kwenye mizozo ya kivta, ripoti ambayo imechapishwa hii leo.

Watoto wa kike wanakuwa hatarini kuozeshwa mapema na wengi wao ni wale wanaotoka familia maskini na makundi ya pembezoni
©UNFPA-UNICEF Nepal/KPanday

Ndoa za utotoni zashamiri Pembe ya Afrika - UNICEF

Watoto wa kike wenye umri mdogo hata miaka 12 huko Pembe ya Afrika wanalazimishwa kuolewa sambamba na kukeketwa au FGM, katika viwango vya kutisha wakati huu ambapo ukame mkali kuwahi kukumba eneo hilo katika kipindi cha miaka 40 ukisukuma familia katika mazingira magumu, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto duniani, UNICEF.

Familia kutoka Eritrea ikiwa kwenye kituo cha muda Romani wakisubiriwa kuhamishwa hadi Netherlands.
© UNHCR/Stefan Lorint

Idadi ya wasaka hifadhi nchi ya tatu kuongezeka 2023

Zaidi ya wakimbizi milioni 2 mwaka ujao WA 2023 watahitaji kuhamishiwa nchi ya tatu ikiwa ni ongezeko kwa asilimia 36 ikilinganishwa na mahitaji ya mwaka huu ambayo ni wakimbizi milioni 1.5 pekee, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR kupitia tathmini ya makadirio ya kuhamia nchi ya tatu kwa mwaka 2022.