Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Somalia

Watoto wakimbizi kutoka Somalia wakiwa kwenye kambi ya wakimbizi ya Daadab nchini Kenya ambako WFP inawapatia misaada ya dharura.
WFP/Rose Ogola

Majanga yanavyozidi kushamiri isiwe kisingizio cha kusigina haki za mtoto- UN

Wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa hususan zile za mtoto wametoa taarifa ya pamoja hii leo huko Geneva, Uswisi wakisema  majanga ya kiafya, kibinadamu na yale  yanayohusiana na tabianchi yakizidi kuongeza changamoto kubwa duniani kila uchao kama vile ukimbizi wa ndani, ukatili wa kingono na njaa, serikali lazima zikumbuke kuwa watoto wana haki kamilifu za kimsingi za kibinadamu na kwamba haki hizo zinapaswa kulindwa.

Wanawake wanasubiri msaada wa chakula katika kituo cha usambazaji huko Afgoye, Somalia.
UN Photo/Tobin Jones

Wanawake na Wasichana ndio wahamiaji wengi zaidi katika Mashariki na Pembe ya Afrika - Ripoti ya IOM 

Wanawake na wasichana wameelezwa kuwa ndio idadi kubwa ya wahamiaji Mashariki na Pembe ya Afrika wakiwa ni asilimia 50.4 ya wahamiaji wote ikilinganishwa na wanaume na wavulana, ambao ni asilimia 49.6, jambo ambalo ni la kipekee katika ukanda huo kwa mujibu wa takwimu za kikanda zilizotolewa leo na ripoti ya shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji (IOM) iliyotolewa leo jijini Nairobi, Kenya.  

Mama na mwanae katika kituo cha afya cha kutibu utapiamlo nchini Somalia
© UNICEF/Sebastian Rich

Hatuwezi kusubiri hadi baa la njaa litangazwe tunafanya kila tuwezalo kuwanusuru Wasomali:WFP 

Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP limekuwa mstari wa mbele nchini Somalia likifanya kila liwezekanalo kufikisha msaada wa kuokoa maisha kwa takriban watu milioni 3.7 walio katika hatihati ya baa la njaa, huku zaidi ya 300,000 miongoni mwao wakipatiwa msaada wa lishe. Hata hivyo shirika hilo limeonya kwamba hatua Madhubuti zisipochukuliwa sasa baa la njaa haliepukiki. Leah Mushi na taarifa zaidi 

Sauti
2'38"
Katika Kaunti ya Turkana nchini Kenya, Abenyo Natiir  (kati- kulia) akitengeneza shanga za urembo akiwa na binti yake Awesit Lisilgor (kushoto- kati)
© UNICEF/Nichole Sobecki

Katikati ya ukame Pembe ya Afrika, bado kuna tumaini la nuru ya kujikwamua

Pembe ya Afrika hali ya ukame inazidi kutishia uwezekano wa baa la njaa kwenye eneo hilo linalojumusha Kenya, Somalia na Ethiopia huku Umoja wa Mataifa ukisema takribani watu milioni 18.4 huamka kila siku bila uhakika wa mlo huku idadi hiyo ikitarajiwa kufikia milioni 20 mwezi ujao wa Septemba. Wanawake na watoto wameathirika zaidi ambapo kando ya njaa wanakumbuka kile walichokuwa wanafanya hali ilivyokuwa nzuri na wanatamani hali hiyo irejee.

Sauti
2'24"