Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Somalia

Geti la kuingia kwenye makao makuu ya ofisi ya haki za binadamu OHCHR mjini Geneva Uswis
UN Photo/Jean-Marc Ferré

Uchunguzi huru na wa haki lazima ufanyike dhidi ya waliokufa Laas Canood: Turk

Kutoka Geneva nchini Uswisi Kamisha Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa , Volker Turk ametoa wito kwa mamlaka ya Somalia kuhakikisha uchunguzi huru unafanyika bila upendeleo kufuatia mauaji yaliyotokea baada ya mapigano makali kuanzia tarehe 5 mwezi huu wa Februari nchini humo kati ya vikosi vya usalama na wanajamii wa ukoo wa Laas Canood.

Wafanyakazi wa IOM wanaosimamia kambi wanafanya kazi katika baadhi ya kambi kubwa za watu waliokimbia makazi yao nchini Somalia.
IOM/Claudia Rosel

Mashirika ya UN yanavyohaha kuwasaidia waathirika wa mizozo na ukame Baidoa Somalia

Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani, WHO inasema idadi ya milipuko ya magonjwa iliyoripotiwa na dharura za kiafya zinazohusiana na tabianchi katika Ukanda wa Pembe ya Afrika zimefikia kiwango cha juu zaidi kuwahi kutokea karne hii, na hivyo kuzidisha janga la kiafya katika eneo ambalo watu milioni 47 tayari wanakabiliwa na njaa kali. 

Sauti
4'27"
Fadumo Ibrahim, mkulima huyu akipalilia shamba lake la mahindi huko Marka, Somalia mwezi tarehe 22 Novemba mwaka 2021.
©FAO/Arete/Abdulkadir Zubeyr.

Msaada kutoka FAO waleta matumaini kwa wakazi wa Hirshabelle nchini Somalia

Ukame wa zaidi ya miongo minne na mafuriko vimekuwa ‘mwiba’ kwa wananchi wa Somalia na hivyo kutishia uhakika wa kupata chakula halikadhalika mbinu za kujipatia kipato. Shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo, FAO kwa msaada kutoka serikali ya Sweden imewezesha mradi wa kusaidia wakulima wadogo kwa kuwapatia pembejeo na msaada wa fedha na sasa kuna nafuu hasa kwenye jimbo la Hirshabelle nchini humo. 

Amira, mwenye umri wa miaka 12 anafanya kazi za shule akiwa kwenye bweni la kituo cha kulinda watoto cha Garisa wasichana nchini Somalia
© UNICEF/UN0657272/Odhiambo

Pembe ya Afrika: UNFPA yazindua ombi la dola milioni 113 kwa wanawake na wasichana walioathiriwa na ukame

Ukame ambao haujawahi kutokea katika Pembe ya Afrika unaathiri jamii nzima, lakini ni wanawake na wasichana ambao wanalipa “gharama kubwa isiyokubalika,” limesema Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu duniani na masuala ya afya ya uzazi UNFPA hii leo wakati likizindua ombi la dola milioni 113.7 ili kukidhi mahitaji yao.

Michael Dunford, Mkurugenzi wa WFP Pembe ya Afrika akihojiwa na UN News.
UN/ Leah Mushi

Hatari ya baa la njaa bado ni jinamizi linaloizonga Somalia: WFP Dunford

Ukame uliolighubika eneo la Pembe ya Afrika kwa miongo minne mfululizo umesababisha changamoto kubwa kwa mamilioni ya raia wa Kenya, Ethiopia na Somalia nchi ambayo maeneo mengi yanakabiliwa na kutokuwa na uhakika wa chakula na hatihati ya kutumbukia kwenye baa la njaa. Mashirika ya misaada ya kibinadamu likiwepo la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP yako mstari wa mbele kuwasaidia watu wenye uhitaji hususani wa chakula.

Sauti
2'