Tubadili mwelekeo wa kukabili uhaba wa chakula- Ripoti
Mtandao wa kimataifa duniani dhidi ya janga la chakula, GNAFC umezindua ripoti yake hii leo huko Roma, Italia kuhusu janga la chakula inayosema kuwa idadi ya watu wanaokabiliwa na ukosefu mkubwa wa chakula sambamba na wanaohitaji siyo tu msaada wa chakula kuokoa maisha yao bali pia msaada wa kuendesha maisha yao inaongezeka kwa kiasi kinachotia mashaka makubwa.