Vitisho dhidi ya haki za binadamu vinaongezeka, halikadhalika suluhisho-Bachelet
Kamishna Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa, Michelle Bachelet hii leo akihutubia mkutano wa 43 wa Baraza la Haki za binadamu mjini Geneva Uswisi amesema vitisho dhidi ya haki za binadamu, maendeleo na amani vinaweza kuwa vinaongezeka lakini pia utatuzi kwa vitendo unaozingatia kaanuni nzuri za haki nao unaongezeka.