Vifaa na misaada kutoka kituo kikuu Addis Ababa vyaleta mabadiliko- WFP
Shirika la mpango wa chakula la Umoja wa Mataifa, WFP, limechukua hatua kuhakikisha kuwa wakati huu wa janga la ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19, vifaa vya matibabu pamoja na wafanyakazi wanaweza kufika popote pale wanapohitajika kwa wakati.