Asilimia 1 ya watu wote duniani wamelazimika kukimbia makwao: UNHCR
Ripoti mpya ya mwenendo wa kimataifa wa wakimbizi na watu waliotawanywa duniani ambayo imetolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR inasema asilimia moja ya watu wote duniani wamelazimika kufungasha virago na kukimbia makwao kwa sababu moja au nyingine.