Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Burundi

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akiwa katika mahojiano maalumu na Mkuu wa Idara ya mawasiliano ya umma ya Umoja wa Mataifa Melissa Fleming mjini New York Marekani Septemba 18, 2019.
UN News/Ben Lybrand

Kutowashirikisha vijana kwenye tabianchi ni janga- Guterres

Kuelekea siku ya kimataifa ya amani ambayo huadhimishwa kila mwaka Septemba 21, leo katika maadhimisho kwenye Umoja wa Mataifa Katibu Mkuu wa Umoja huo, Antonio Guterres ametoa wito wa hatua madhubuti kuchukuliwa kukabiliana na changamoto kubwa za dunia ikiwemo mabadiliko ya tabianchi ili kudumisha amani kwa wote. 

Sauti
3'12"
Hapa Koula, jimbo la Kivu Kusini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambapo watot waliorereja makwao wakiwa nje wakifuatilia darasa. Mzozo wa kivita jimboni humo umesabababisha wakazi wake kukimbilia na kusaka hifadhi kwingineko.
OCHA/Naomi Frerotte

Hata nikikata pumzi sasa kile nimefanya kimetosha- Mshindi wa Nansen Afrika 2019

Mshindi wa tuzo ya wakimbizi ya Nansen kwa kanda ya Afrika kwa mwaka huu wa 2019 Evariste Mfaume, amesema hata siku akikata pumzi, kile ambacho ameweza kufanya kuleta utangamano kati ya wakimbizi na wananchi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kitakuwa kimetosha. Tuzo hiyo ya Nansen hutolewa na shirika la kuhudumia wakimbizi duniani,  UNHCR.

Sauti
2'5"
Wakimbizi wa Burundi wanaorejea nchini mwao kutoka Tanzania wakiwa kwenye kituo cha mpito cha Mabanda katika jimbo la Makamba nchini Burundi. (24 Aprili 2018)
OCHA/Christian Cricboom

Kuna hali ya hofu na vitisho nchini Burundi- COIB

Ikiwa imesalia chini ya mwaka mmoja kuelekea kufanyika uchaguzi wa rais,wabunge na serikali za mitaa nchini Burundi mwakani 2020, kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuichunguza Burundi COIB imetoa ripoti yake hii leo mjini Geneva Uswisi na kusema kuwa kuwa kuna hali ya hofu na vitisho kwa watu wote ambao hawaonyeshi kukiunga mkono chama tawala cha CNDD-FDD. Grace Kaneiya na ripoti kamili.

Sauti
2'21"