Je wajua nchi inayoongoza kuwa na wakimbizi wengi? na taifa linalohifadhi wakimbizi wengi zaidi duniani?
Takwimu za mpaka mwishoni mwa mwaka 2020 zilizotolewa na Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Wakimbizi UNHCR zinaonesha duniani kote kuna jumla ya wakimbizi milioni 82.4.
Takwimu hizi huenda zikaongezeka mwaka huu kwa kuwa janga la Corona au COVID-19 limesababisha watu wengi kuyakimbia makazi yao.