Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Nchi 1 kati ya 8 ndio zenye mipango ya kulinda wanawake dhidi ya athari za COVID-19: UN
Takwimu mpya zilizotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya wanawake UN Women na lile la mpango wa maendeleo UNDP kuhusu hatua za kimataifa za kukabiliana na janga la corona au COVID-19 katika suala la kijinsia zinaonyesha kwamba mikakati ya hifadhi ya jamii na masuala ya ajira wakati wa janga hili imeyapa kisogo mahitaji ya wanawake.
Yemi Alade: Niko tayari kujitolea kwa nguvu zangu zote kufanikisha malengo ya UNDP
Mwanamuziki Yemi Alade, raia wa Nigeria ambaye hivi karibuni ametangazwa kuwa Balozi mwema wa shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo UNDP amesema malengo ya UNDP yanaendana na malengo yake kwa hivyo atajitolea kwa uwezo wake wote. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.
Afrika, hatua tulizochukua dhidi ya COVID-19 zimedhihirishia ulimwengu uthabiti wetu.
Fikra za baadhi ya watu kuwa maelfu kwa maelfu ya watu barani Afrika watapukutika kutokana na janga la ugonjwa wa Corona, au COVID-19 zimekuwa ndivyo sivyo baada ya bara hilo kuchukua hatua kitaifa na kikanda na hatimaye hadi sasa kudhihirisha umuhimu wa mshikamano katika kukabili adui. Hilo limebainishwa wakati wa hotuba za marais waliohutubia mjadala mkuu wa mkutaon wa 75 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwa njia ya mtandao kutokana na vikwazo vilivyopo Marekani kutokana na janga la Corona.
Hatua tulizochukua dhidi ya COVID-19 zimedhihirishia ulimwengu uthabiti wetu Afrika
Fikra za baadhi ya watu kuwa maelfu kwa maelfu ya watu barani Afrika watapukutika kutokana na janga la ugonjwa wa Corona, au COVID-19 zimekuwa ndivyo sivyo baada ya bara hilo kuchukua hatua kitaifa na kikanda na hatimaye hadi sasa kudhihirisha umuhimu wa mshikamano katika kukabili adui. Hilo limebainishwa wakati wa hotuba za marais waliohutubia mjadala mkuu wa mkutaon wa 75 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwa njia ya mtandao kutokana na vikwazo vilivyopo Marekani kutokana na janga la Corona. Flora Nducha anamleta Assumpta Massoi ambaye amefuatilia hotuba za viongozi hao na anaeleza kwa kina.
Niko tayari kujitolea kwa nguvu zangu zote kufanikisha malengo ya UNDP-Yemi Alade
Mwanamuziki Yemi Alade, raia wa Nigeria ambaye hivi karibuni ametangazwa kuwa Balozi mwema wa shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo UNDP amesema malengo ya UNDP yanaendana na malengo yake kwa hivyo atajitolea kwa uwezo wake wote.
Ushirikiano wa ndani na wa kimataifa umetusaidia-Rais Farmajo wa Somalia
Rais wa Somalia Mohamed Abdullahi Mohamed Farmajo hii leo akihutubia mjadala wa wazi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwa njia ya video iliyorekodiwa, amesema wanaendelea kushirikiana na Umoja wa Mataifa na wadau wengine katika masuala mbalimbali ili kutengeneza mstakabali mzuri kwa watu wa Somalia.
Ushirikiano wa kimataifa umeshindwa kukidhi haja wakati wa COVID-19:Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameliambia Baraza la Usalama hii leo kwamba ushirikiano wa kimataifa umeiangusha dunia na kushindwa kukidhi haja wakati huu wa janga la corona au COVID-19 na hivyo ametoa wito wa kutafakari kwa kina kuhusu suala la utawala wa dunia na ushirikiano wa kimataifa.
Hakuna nchi hata moja inaweza peke yake kumudu janga kama hili la COVID-19
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya hii leo akihutubia mjadala wa wazi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwa njia ya vdeo iliyorekodiwa kutokana na janga la virusi vya corona kutoruhusiu viongozi wa dunia kukutana New York Marekani kama ilivyo ada ya kila mwaka, ameueleza ulimwengu kuwa ugonjwa wa COVID-19 linapaswa kutoa msukumo mpya, “kwa juhudi zetu za pamoja za kuimarisha ushirikiano wa kimataifa.” Na hakuna nchi ambayo peke yake inaweza kumudu janga kubwa la kiwango cha COVID-19.
Taarifa potofu ziliongeza changamoto katika kukabili Corona
Umoja wa Mataifa na wadau wamezisihi nchi zote duniani kushughulikia kile walichoekelea kuwa ni janga la taarifa ambalo limeibuka kutokana na janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19, katika ulimwengu wa kawaida na mtandaoni.
UN iko tayari kuyasaidia mataifa yasiyo na bahari, kujikwamua na COVID-19
Mfumo wa umoja wa Mataifa umesema unashikamana na mataifa yanayoendelea yasiyo na bahari ambayo yanakosa fursa muhimu za viunganishi vya biashara na kuyasaidia katika juhudi zao za kujijenga upya pindi janga la corona au COVID-19 litakapokwisha.